Serikali ya Malaysia imeweka tangazo magazetini,ikitafuta mmiliki wa
ndege tatu aina ya Boeing 747 ambazo zimeachwa katika uwanja wa ndege Kuala
Lumpur.
Tangazo hilo lililotolewa na
mamlaka ya viwanja vya ndege,limeonya mmiliki wa ndege hizo kwamba akikosa
kwenda kuzidai katika kipindi cha siku 14 zijazo, basi watakuwa na haki ya
kuziuza au kuzitumia kwa namba nyingine.
Mamlaka hiyo imesema ndege
hizo pia hazijalipiwa ada ya kutua na ada ya maegesho.
Amesema kwa miongo kadha sasa
kuna ndege ambazo zimekuwa zikiachwa uwanjani lakini sana huwa ni ndege ndogo.
Moja iliyoachwa miaka ya 1990
iliuzwa na baadaye ikaanza kutumiwa kama mgahawa katika kitongoji kimoja cha
mji wa Kuala Lumpur.
Maafisa wanasema malipo yasipopokelewa
kufikia Desemba 21,ndege hizo zitapigwa mnada au ziuzwe zitumiwe kama vyama
vikukuu kulipa gharama.
0 comments:
Post a Comment