Thursday 22 October 2015

Je Aspirin inazuia kurejea kwa Saratani…..?

Utafiti mkubwa na wa kwanza kubaini iwapo umezaji wa tembe za Aspirin kila siku unapunguza kwa kiwango kikubwa athari ya kurejea kwa saratani umeanza nchini Uingereza.

Jaribio hilo litahusisha watu 11,000 wanaotibiwa ama waliomaliza matibabu ya aina tofauti za saratani.
Utafiti huu utakaoendelea kwa kipindi cha hadi miaka 12, utatathmini matokeo ya kumeza miligram 300 ya Aspirin kila siku na kutofautisha na kundi lingine litakalokuwa likimeza miligramu 100 ya dawa hiyo.
Makundi hayo mawili yatalinganishwa na kundi la tatu, ambalo litakuwa likimeza dawa ghushi.
Iwapo utafitu huu utabaini kuwa kweli Aspirin inapunguza athari ya kurejea kwa maambukizi ya saratani, basi hii itachochea mwamko mpya katika matibabu ya Saratani ambayo kwa kawaida hugharimu kiasi kikubwa cha pesa.
Majaribio hayo yataendeshwa katika vituo 100 nchini Uingereza kwa kipindi cha hadi miaka 12 kuanzia leo.
Hata hivyo onyo limetolewa kuwa, Aspirin haifai kutumika na kila mtu bila ya ushauri wa daktari.

Hii ni kwa sababu uchunguzi tofauti ulibaini kuwa umezaji wa dawa hiyo ya Aspirin, husababisha vidonda vya tumbo na pia uvujaji wa damu akilini, kwa sababu viungo vilivyo kwenye tembe hizo za Aspirin husababisha damu kuwa maji maji (Nyepesi)

0 comments:

Post a Comment