Thursday 22 October 2015

Je wajua siri ya Mamba usingizini….?

Wataalamu wa masuala ya wanyama wamegundua kwamba, mamba ana uwezo wa kulala huku jicho lake moja likiwa wazi.

Utafiti huo ambao umewaacha wengi wakishangaa, kwani picha nyingi duniani huonyesha kuwa mamba hulala fofofo, wakati jicho lake moja huwa likiona.
Wanasema hilo hufanyika kwa sababu sehemu moja ya ubongo wa mamba huwa imezima, ilihali sehemu nyingine ikifanya kazi.
Wanasayansi wamebainisha kwamba kusinzia kwa jicho moja ni jambo la kawaida kwa baadhi ya ndege, kama vile pomboo ambao huendelea kuangalia kwa nusu ya ubongo wao , wakati nusu nyiongine ya ubongo ikiwa imepumzika .

Utafiti huo ulichapishwa katika jarida majaribio ya kibaiolojia

0 comments:

Post a Comment