Friday 9 October 2015

Utafiti waonesha hatari ya sigara,China……

Utafiti mpya umeonya kuwa sigara ina uwezo wa kuua kijana mmoja kati ya vijana watatu nchini China.

Hali hiyo itatokea kama hapatakuwa na hatua yeyote itakayofanyika itakayowafanya waache tabia hiyo.
Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Lancet linalohusiana na masuala ya tiba, unasema kuwa China inakabiliwa na ongezeka kubwa la vifo vya mapema, kwa kuwa theluthi mbili ya vijana nchini humo huanza kuvuta sigara wakiwa chini ya miaka ishirini.
Na karibu nusu hufa kutokana na tabia zao. Hivyo kama hali ya sasa itaendelea utafiti unaainisha kuwa idadi ya watu wanaokufa kutokana na matumizi ya tumbaku kila mwaka nchini China yataongezeka, wengi wao wakiwa ni wanaume ambapo watafikia watu milioni mbili ifikapo mwaka 2030.

Wanasayansi walifanya tafiti mbili kwa nchi nzima ndani ya miaka kumi na tano ukiachilia mbali ufuatiliaji wa athari za kiafya kutokana na uvutaji sigara nchini China.

0 comments:

Post a Comment