This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Friday, 13 March 2015

Idadi ya mimba za utotoni yaongezeka..!!!!!

Msichana mmoja kati ya wanne wenye umri wa miaka 15 hadi 19 ni mjamzito au ana mtoto imeelezwa. Idadi hii inawakilisha maisha halisi na kuonesha kwamba kama jitihada za makusudi hazitachukuliwa, wasichana wataendelea kukosa haki zao za msingi na kuzidi kuwa wategemezi. Hayo yalisema na mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa utafiti katika ukunga, ulioandaliwa na LUGINA Afrika Midwives Research Network (LAMRN) uliofanyika katika Hoteli ya Kunduchi jijini Dar es Salaam. Mama Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),amesema vifo vya akinamama wajawazito na watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano,ni tatizo katika nchi zote zilizopo Kusini mwa Bara la Afrika hata hivyo jitihada mbalimbali zinafanyika ili kuhakikisha tatizo hilo linapungua au kumalizika kabisa. Kuhusu mimba za utotoni Mwenyekiti huyo wa WAMA, amesema tafiti zilizofanyika zinaonesha wasichana wanaanza kufanya mapenzi mapema zaidi wakiwa na umri mdogo, ukilinganisha na wavulana jambo linalopelekea kupata mimba za utotoni na hivyo kukosa elimu kwa kukatisha masomo yao

Mtoto akatwa uume kimakosa akitahiriwa...

Mtoto aitwaye Badru Muhidin mwenye umri wa miaka miwili, amepata pigo kubwa baada ya kukatwa uume wake kimakosa na babu yake aliyekuwa amempeleka kutahiriwa kienyeji huko Mbagala jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Mama mzazi wa mtoto huyo Mwajuma Hussein ambaye ni mkazi wa Yombo jijini Dar, amesema aliishi na mwanaye peke yake bila baba yake kwani walitengana Juni mwaka jana baada ya kuishi bila kufunga ndoa kwa muda mrefu, lakini mara kwa mara alikuwa akimpeleka mwanaye nyumbani kwa wazazi wa mumewe kuwasalimia. Amesema baada ya kumkuta katika hali hiyo, alianza kuhangaika naye hospitalini kutafuta msaada, alipofika Temeke aliambiwa na madaktari kwamba kijana wake alikatwa vibaya na hivyo analazimika kufanyiwa upasuaji ili kumnusuru. Babu wa mtoto huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kufunguliwa shauri katika Kituo cha Polisi Mbagala Kizuiani kwa madai ya ukatili.

Mchungaji amsaliti mchungaji mwenzake....

Matukio ya watumishi wa Mungu kukutwa na skendo za udhalilishaji imekua ikitokea, kama ikitokea huwa inakuwa stori ambayo watu wengi wanazipa uzito zaidi kutokana na kwamba inajuwa ishu ambayo inahusisha watumishi wa nyumba za ibada. Kutoka Nigeria chukua hii story Mchungaji mmoja kaamua kumpa mke wake talaka kutokana na kugundua kuwa mke wake ana uhusiano na mchungaji mwenzake ambaye ni rafiki yake wa karibu pia. Mchungaji Jack aliiambia Mahakama ya Lagos, Nigeria kwamba mkewe Kate,aligundulika kuwa na uhusiano na mchungaji huyo baada ya kuihama nyumba yake tangu mwaka 2011 na hajawahi kurudi tena. Hata hivyo Kate hakuweza kuhudhuria Mahakamani hapo kusikiliza kesi hiyo,hivyo kesi ikaahirishwa hadi March 23 itakaposikilizwa tena Mahakamani hapo.

Twitter kuzuia picha za utupu wa kisasi.....

Mtandao wa Twitter umebadili sheria zake katika kuzuia watumiaji wake kuchapisha Picha na video chafu. Sheria ya mtandao huu wa kijamii inasema ''Marufuku kuchapisha picha au video chafu zilizopigwa au kurekodiwa kisha kusambazwa bila ridhaa ya muhusika aliye kwenye video na picha hizo'' Mwezi uliopita vitendo hivi vilitambulika kuwa makosa ya jinai uingereza na Wales. Msemaji wa Kampuni ya Twitter amesema watumiaji watakaobainika kukiuka masharti mapya ''Anuani zao zitafungiwa'' Watumiaji wanaopeleka malalamishi Twitter kuhusu picha na Video zilizochapishwa watatakiwa kujitambulisha na kuithibitishia Kampuni kuwa hawakuwahi kutoa idhini ili kuchapisha picha au video mtandaoni na kuonekana kwa hadhira.

Wednesday, 11 March 2015

Mwandishi aporwa mbele ya Camera..

Mwandishi maarufu wa runinga kutoka Afrika Kusini ameibiwa hadharani alipokuwa akijiandaa kwenda hewani mbele ya kamera. Kanda ya video imewaonyesha wanaume wawili wakimvamia Vuyo Mvoko, kutoka yuninga ya taifa ya SABC ambaye alikuwa nje ya hospitali moja ya mjini Johannesburg akiripoti kuwasili kwa rais wa Zambia ili kufanyiwa ukaguzi wa matibabu. Bwana Mvoko baadaye alisema kuwa mmoja wa wezi hao alimtishia na bunduki alipokataa kumpa simu yake ya rununu. Wezi hao walionekana kutojali kamera zilizokuwa mbele yao. ''Sikuelewa ni kwa nini waliweza kunivamia mbele ya Kamera ilihali taa zote zilikuwa zikiwaka na kamera zilikuwa zikinasa kila kitu na, waliona kilichokuwa kikiendelea''. Baada ya mda mfupi bwana Mvoko ambaye ni mhariri wa kituo hicho cha habari alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter akisema kuwa yuko salama salmin na kutuma kanda ya video hiyo mtandaoni. Maafisa wa polisi wanasema kuwa wezi hao waliiba laptopu, na simu na kwamba maafisa walikuwa tayari wanachunguza kisa hicho.

Mh.Bendera aagiza uchunguzi kugundua chanzo cha moto kuunguza migodi Mererani

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Manyara imetembelea katika migodi iliyoteketea kwa moto katika machimbo ya Tanzanite Mirereani Simanjiro huku mkuu wa mkoa huo Joel Bendera akiwaagiza wataalam wa Tanesco idara ya madini na jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa haraka kugundua chanzo cha moto huo ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakao bainika. Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa aliongozana na wataalam wa Tanesco idara ya madini na vyombo vya ulinzi na usalama ambapo kabla ya kuzungumza na wananchi alitoa nafasi kwa waathirika kutoa madukuduku yao nawo waliendelea kulalamikia uzembe uliyofanyika katika tukio ilo na kuendelea kusisitiza kuwa kuna hujuma katika tukio ilo na wengine wakilalamikia njaa na mazingira magumu ya kulala. Akitoa maelezo ya awali mkuu wa wilaya ya Simanjiro Mahamud Kambona ameeleza namna tukio ilo lilivyo waathiri wachimbaji wadogo na hatua za awali walizochukua. Ukafika wakati wa mkuu wa mkoa wa Manyara Dk Joel Bendera kutoa pole kwa niaba ya serikali na kuviagiza vyombo vinavyo husika kufanya uchunguzi wa kina kwa haraka ili kujuwa kama ilikuwa ni ajali ya kawaida au ni hujuma huku mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa Manyara Christopher Fuime akitoa angalizo kwa wachimbaji wadogo kuhusu uhifadhi na matumizi ya mulipuko.

Serikali ya Tanzania kuwaonyesha ukali wauaji wa watu wenye albinism...

Utashi wa kisiasa upo ili kukemea ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino,amesema Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana, baada ya Ofisi ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa kuziomba serikali za Tanzania, Malawi na Burundi kuchukua hatua za kusitisha mauaji hayo. Bi Chana amesema hatua ya kwanza itakayochukuliwa na serikali ya Tanzania ni kuwapatia wahalifu wa mauaji hayo adhabu kali, ikiwemo hukumu ya kifo, hata kama Tanzania haijatekeleza adhabu hiyo kwa muda mrefu. Kadhalika amesema kama nchi nyingine zinzvyochukua hatua dhidi ya ugaidi, serikalia ya Tanzania ina haki ya kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vya mauajia ya albino. Hatimaye ametoa wito kwa watanzania wote waonyeshe ubinadamu na huruma ili kukomesha ukatili huo ambao ni kinyume na haki za binadamu.

Tuesday, 10 March 2015

LISSU ATANGAZA RASMI ZITTO SI MWANACHADEMA TENA

Mwanasheria mkuu wa chama cha upinzani nchini CHADEMA, Tundu Lissu leo ametangaza kuvuliwa uanachama kwa mbunge wa Kigoma Kasikani Zitto Kabwe baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaamkutupilia mbali pingamizi la mbunge huyo la kuzuia asijadiliwe. "Kwa mujibu wa katiba ya chama cha CHADEMA, mwanachama yoyote anapofungua kesi mahakamani dhidi ya chama chake, endapo atashindwa katika kesi hiyo atakuwa amejiondoa uanachama wake, kwahiyo natangaza rasmi rasmi Zitto Kabwe sio mwanachama tena wa Chadema. Kwa upande wake Zitto Kabwe amesema hawakuwa na wito wa mahakamani leo na Jaji wa kesi kahamishiwa Tabora na hawana taarifa ya Jaji Mpya, pia kaongeza kuwa Mwanasheria anafuatilia na atatoa statement. Licha ya kutupilia mbali kesi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe, Mahakama kuu imemtaka kulipa gharama zote za kesi toka ilivyoanza. Mwaka jana Zitto Kabwe aliweka pingamizi mahakamni kuzuia kikao cha Kamati Kuu kumjadili na hoja yake ilikuwa ni kupinga kuitisha kamati kuu kabla shauri lake kusikilizwa na Baraza Kuu

Apple yaja na Saa za kisasa..

Kampuni ya Apple imezindua saa ya kisasa ambayo inauwezo wa kupiga simu,kupokea barua pepe,kucheza muziki na kufuatilia masuala ya afya na mazoezi. Kampuni ya Apple Inc itaanza kuuza saa zake mpya mnamo mwezi April 24 mwaka huu, na bei ya kuanzia sokoni itakuwa dola 10,000 ama paundi 6,611 na bidhaa yake ya kwanza ghali ilitolewa miaka mitano iliyopita katika malengo ya kuongeza wigo wa bidhaa zake hasa vifaa vya simu za mkononi. Sasa hiyo kutoka kampuni ya Apple ya kimichezo kwa zile ndogo zina milimita thelathini na nane itauzwa kwa dola 349 na saa kubwa itauzwa kwa dola 549 na bidhaa ya mwisho itauzwa kwa dola elfu kumi ,hii ni kwa muujibu wa Afisa mtendaji wa kampuni hiyo , Tim Cook said mapema wiki hii.

Mahaka Ivory coast yamhukumu Mke wa Gbagbo miaka 20 gerezani

Mahakama nchini Ivory Coast imemhukumu aliyekuwa mke wa Rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kifungo cha miaka 20 gerezani. Simone Gbagbo amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kushiriki katika ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi nchini humo mwaka 2010 na 2011. Simone Gbagbo alikamatwa mwaka 2011 pamoja na mume wake, aliyekuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama ya uhalifu mjini The Hague Uholanzi. Katika ghasia hizo watu takriban elfu tatu walifariki dunia.

Monday, 9 March 2015

Mtoto mwingine Albino akatwa mkono,Waganga wasema vinavyotumika kishirikina..

Matukio ya ukatili dhidi ya albino yanaendelea kuwa tishio nchini,baada ya mtoto wa miaka sita kukatwa kiganja cha mkono Shambulio hilo jipya limetokea mkoani Rukwa kusini magharibi mwa nchi hiyo, ambapo usiku wa kuamkia jana watu wasiojulikana walimshambulia na kumkata kiganja mtoto mwenye umri wa miaka sita, Baraka Cosmas na kisha kutokomea nacho kusikojulikana. Tukio hilo lililotokea katika kijiji cha Kipeta Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga,ambako mtoto huyo anaishi na wazazi wake, Cosmas Yoram (32) na Prisca Shaaban. Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Jacob Mwaruanda,amesema tukio hilo ni la saa 8 usiku wa kuamkia Jumapili wakati mtoto huyo akiwa amelala na mama yake huku Baba wa mtoto huyo hakuwepo wakati huo. Mkurugenzi wa shirika linalotetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi la Under The Same Sun Vicky Mketema,amezungumzia jinsi ukatili huo unavyofanyika. Na kwanza ameanza kwa kuzungumzia kwa uapnde wa watu ambao wanataka kupata madini,kuwa wanaamini kuwa mguu wa albino unaweza kuwa msaada kwao kufanikiwa katika hilo,msikie hapa chini. https://soundcloud.com/wilberd-kiwale/wanga-wasema-viungo-vya-albino-vinavyotumika

Ngoma ya Odeo ft vocaliser-Ngakukunda Hiii Hapaaa..

Kijana toka mkoani kIlimanjaro anafahamika na wengi kama Odeo hapa nakuwekea link ya kuipata ngoma yake mpya,kamshirikisha kijana mwingine anaekuja vizuri kwenye game anafahamika kama vocaliser. Bofya HAPA https://mkito.com/song/ngakukunda-ft-vocaliser/12897 simu no: +2557565727571

Hii kalii Kondom Zatumika Kama Fasheni za Nywele

Kila kukicha kumekuwa na mambo mapya katika jamii inayotuzunguka na kutokana na utandawazi umetufanya tuone na kujua kila kinachoendelea katika ulimwenguni huu wa sayansi na teknolojia. Kwa sasa kumekuwa na mitindo mbalimbali ya fashion kama kwenye nguo, makeup, viatu na kubwa zaidi kuhusu hii style mpya hapa mjini ya kila mtu kuweka dread kwa namna yake, sasa mama moja wa makamo na raia wa Ghana alitoa mpya baada ya nywele zake kuzivisha kondomu kwa kuzifunga kama dreadlock. Unaionaje hiyo Styl????

Utafiti:Matumizi ya Paracetamol ni hatari kwa Afya..!!!

Matumizi ya kila siku ya dawa za kupunguza maumivu za paracetamol huongeza hatari ya ugonjwa wa moyo,kiharusi na kufupisha maisha ya binadamu, utafiti mpya umeonya. Paracetamol hupendelewa zaidi na madaktari wengi hudai zi salama kulinganisha na aspirin, ambayo imehusishwa na kuvuja damu tumboni na ibuprofen iliyohusishwa na magonjwa ya moyo na kiharusi. Lakini watafiti wa Uingereza waliofanya uchunguzi huo uliowahusisha wagonjwa 666,000 wanasema hatari iliyomo katika dawa hizo,huenda ilipuuzwa na sasa wameagiza uchunguzi ufanywe kuhusu usalama wake. Taarifa hizo iwapo ni za uhakika, itakuwa pigo kwa wengi kwa vile paracetamol zimezoeleka kuliko dawa nyingine yoyote ile ya kupunguza maumivu, na inapatikana kirahisi na kila mahali. Zaidi ya hayo makasha milioni 200 ya paracetamol huuzwa kila mwaka. Hata hivyo Prof. Philip Conaghan wa Taasisi ya Dawa ya Rheumatic and Musculoskeletal mjini Leeds Uingereza, amefichua kuwa matumizi ya muda mrefu ya paracetamol yana athari mbaya kiafya. Professa Conaghan alipitia tafiti nane zilizofanyika huko nyuma, kutathimini uhusiano baina ya matumizi ya muda mrefu ya paracetamol na matatizo ya kiafya kwa watu wazima.
Utafiti huo umebaini wagonjwa wanaopewa dawa hizo za kupunguza maumivu mwilini kwa muda mrefu,wana hatari kubwa ya asilimia 63 kufupisha maisha yao. Hatari ya kupatikana ugonjwa wa moyo na kiharusi iko juu kwa asilimia 68, huku pia kukiwa na hatari kubwa ya asilimia 50 ya kupatikana vidonda vya tumbo au hata kuvuja damu. Watafiti hao walihitimisha kuwa kutokana na ukubwa wa matumizi ya paracetamol na urahisi wa upatikanaji, uchunguzaji wa athari zinazoweza kupatikana kutokana na dawa hizo ulipuuzwa. Una maoni gani juu ya utafiti huu??

Waumini wakatwa sehemu zao za siri ili wamuone mungu!..!!!

Ishu ya imani ni ya mtu binafsi na kila mtu ana uwezo wa kuamini kile anachoona ni sahihi kwa mtazamo wake na mtu anapotokea kumuamini kiongozi wake wa dini kwa asilimia kubwa hutekeleza yale anayofundishwa. Sasa hii ya leo inamuhusu mhubiri maarufu wa dini India ambaye ana wafuasi zaidi ya milioni hamsini duniani Gurmeet Ram Rahim Singh anakabiliwa na mashtaka ya kusababisha majeruhi kwa tuhuma za kuwashawishi wafuasi wake 400 kukata sehemu zao za siri ili waweze kuwa karibu na Mungu.
Wafuasi wa Singh walikata sehemu zao za siri kwenye Hospitali ambayo yeye anaimiliki,ambapo kwenye headlines nyingine mhubiri huyu amekuwa akihusishwa na mauaji ya mwandishi wa habari za uchunguzi pamoja na kutuhumiwa kwa unyanyasaji wa kijinsia lakini hajawahi kushtakiwa. Mmoja wa wafuasi wake Hans Raj Chauhan,aliwaambia Polisi kwamba alikatwa sehemu zake za siri kwa sababu alidhani asingetakiwa kwenye jamii kama angekataa kutekeleza utaratibu huo ulioanzishwa Singh. Singh aliwaambia wafuasi wake kwamba wale ambao wanaotekeleza amri hiyo watakuwa na uwezo wa kumuona Mungu. Vipii wewe unaweza kuwa muumini wa hii dini??