Wataalamu
wa jiolojia wameitwa kufanya uchunguzi, ni jinsi gani ardhi ilipasuka na kumeza
magari 12 katika maegesho ya magari jijini Mississippi.
Shimo kubwa la urefu wa futi 400
(120m) na upana wa futi 35 (11m), lilitokea baadaye Jumamosi katika eneo la
Meridian karibu na barabara kuu ya Alabama.
Eneo hilo limekuwa likipokea mvua
kubwa katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, kwa mujibu wa gazeti la
Meridian Star.
Hakuna aliyejeruhiwa katika kisa
hicho, na wahandisi wanatarajiwa kudadisi uthabiti wa ardhi eneo hilo leo.
Bw Buck Roberts kurugenzi wa
usalama wa umma eneo la Meridian, aliambia gazeti hilo kwamba hilo halionekani
kuwa shimo la kawaida, ambalo hutokana na sehemu inayohifadhi maji chini ya
ardhi kukauka na ardhi kuporomoka.
0 comments:
Post a Comment