Tangazo lake linakuja juma moja tu baada ya Mahakama
ya nchi hiyo kuwapa idhini watu wanne tu kukuza bangi kwa matumizi yao ya
kibinafsi.
Rais anasema kuwa watalaamu sasa wanafaa kuja pamoja, ili
kujadili hatma ya baadaye ya uidhinishwaji wa bangi nchini Mexico.
Amesema anahisi madaktari, wasomi na pia wanasoshiolojia
wanapaswa kutoa mchangao wao katika mjadala huo.
Mexico ni moja wa mataifa yaliyoathirika vibaya na ghasia
zinazotokana na magenge ya walanguzi wa madawa ya kulevya.
Vilevile baadhi ya wadau wanashauri kuwa,kuhalalishwa kwa
bangi na mihadarati Mexico na Marekani, kutawaondoa walanguzi wa madawa ya
kulevya kwenye biashara hiyo, na hivyo kupunguza idadi ya watu wanaouawa katika
vita dhidi ya ulanguzi.
0 comments:
Post a Comment