Raia
nchini New Zealand wawanapiga kura kuchagua bendera, ambayo huenda ikachukua
nafasi ya bendera ya sasa.
Kura hiyo ya maamuzi itapigwa
kuanzia leo Novemba 20 hadi Desemba 11, kupitia posta kuamua bendera moja kati
ya tano zilizopendekezwa ambayo ni bora zaidi.
Kutafanyika kura nyingine mwaka
2016 kuamua iwapo bendera mpya itakayochaguliwa kwenye kura ya kwanza, inafaa
kuchukua nafasi ya bendera ya sasa ambayo huwa na bendera ya Uingereza
almaarufu Union Jack.
Waziri Mkuu John Key amesema kuwa,bendera
ya sasa haiakisi New Zealand ya sasa.
Aidha anaamini inafanana sana na bendera
ya Australia, lakini amekiri kwamba ishara zinaonyesha huenda raia wengi wa New
Zealand wakaamua kusalia nayo.
Bendera hizo zimewekwa maeneo mengi kote nchini humo kwa
raia kujionea na kufanya uamuzi.
Aidha zinatolewa bure kwa watu na
makundi ya kijamii yenye milingoti mitano ya kuzipeperushia.
0 comments:
Post a Comment