Mamlaka
kuu inayosimamia upangaji wa uzazi nchini Uchina, imeonya wanandoa nchini humo
kwamba sharti waendelee kutii agizo la kuwa na mtoto mmoja kwenye familia hadi
sheria ifanyiwe marekebisho mwezi Machi.
Alhamisi ya wiki iliyopita serikali
ilitangaza kwamba, ingelegeza sheria na kuwaruhusu
wanandoa kuzaa watoto wawili.
Ilisema uamuzi huo
ulifanywa kutokana na ongezeko kiwango cha wazee, ukilinganisha na vijana
katika jamii na lengo ni kuimarisha uchumi.
Lakini maafisa wamesema
sera ya kuwa na mtoto mmoja katika familia, itaendelea kutekelezwa hadi sharia
ifanyiwe mabadiliko.
Mnamo Ijumaa afisa mmoja
alinukuliwa akisema kwamba wajawazito walio na mimba ya watoto wa pili
hawataadhibiwa tena, jambo lililodokeza kwamba sera hiyo tayari ilikuwa imeanza
kutekelezwa.
Lakini Jumapili Tume ya
Kitaifa ya Afya na Upangaji Uzazi, ilisema maafisa wa serikali wataendelea
kutekeleza sheria hizo hadi sheria ifanyiwe marekebisho Machi.
Serikali inakadiria kwamba
familia 90 milioni zitapata nafasi ya kuongeza mtoto mwingine, sera ya kuwa na
watoto wawili ikianza kutekelezwa.
0 comments:
Post a Comment