Mkuu
wa shirika la kupambana na dawa za kulevya Indonesia, amependekeza mamba
watumiwe kulinda wafungwa waliohukumiwa kunyongwa.
Budi Waseso anataka taifa hilo
lijenge gereza kwenye kisiwa na kizingirwe na mamba akisema wanyama hao ni
walinzi bora kushinda wanadamu, kwani hawawezi kuhongwa.
Amesema atazuru maeneo mbalimbali
katika taifa hilo kutafuta mamba wakali zaidi.
Indonesia ina moja ya sheria kali
zaidi za kupambana na dawa za kulevya duniani, na ilianza tena kunyonga watu
baada ya kusitisha hukumu hiyo kwa miaka mine 2013.
Mpango huu bado umo katika hatua
za mwanzo mwanzo,na bado haijaamuliwa gereza hilo litakuwa wapi na ni lini
litafunguliwa shirika la habari la AFP limesema.
0 comments:
Post a Comment