Wapiga
kura katika jimbo la Ohio nchini Marekani, wamekataa pendekezo la kuhalalisha
matumizi ya bangi katika jimbo hilo.
Pendekezo hilo lililopewa jina
Issue 3, lingefanyia marekebisho sheria ya jimbo la Ohio na kuifanya bangi kuwa
halali kwa raia yeyote aliye na umri wa miaka 21 na zaidi, kuitumia kwa sababu
za kibinafsi na za kimatibabu.
Kuhalalishwa kwa bangi
kungewezesha bidhaa zilizotiwa bangi, kama vile peremende kuuzwa madukani.
Raia wa kawaida pia wangeruhusiwa kukuza hadi mimea minne
ya bangi majumbani.
Lakini kwa mujibu wa makadirio ya
kura yaliyofanywa na vyombo vya habari jimboni humo, pendekezo hilo limeshindwa
na kiwango cha kura mbili kwa moja.
Makundi yaliyotetea kuhalalishwa
kwa bangi yalitumia hadi $12m kwenye matangazo kabla ya kura hiyo kupigwa
Jumanne.
Sheria ya Issue 3 ingetoa idhini
kwa bangi kukuzwa katika maeneo 10 jimbo la Ohio, jambo ambalo wakosoaji
wanasema lingepelekea kuwepo kwa ukiritimba.
Kambi ya waliotetea sheria hiyo
ilikuwa na watu mashuhuri wakiwemo msanii Nick Lachey, na Woody Taft, ambaye ni
ndugu wa rais wa zamani wa Marekani William Howard Taft.
Pendekezo hilo lilipingwa vikali na hospitali
zinazoshughulikia watoto, baadhi ya mashirika ya kibiashara na wakulima.
Majimbo ya Colorado, Washington,
Oregon na Alaska, pamoja District of Columbia, yamehalalisha matumizi ya bangi
kwa sababu za kujiburudisha.
Majimbo 20 nayo huruhusu matumizi
ya bangi kwa sababu za kimatibabu.
0 comments:
Post a Comment