Monday 2 November 2015

Mji uliozoea kupandisha bendera nusu mlingoti mkazi akifa…

Mji mmoja kaskazini mwa Iceland, umekuwa kipeperusha bendera ya taifa nusu mlingoti kila mkazi wa mji huo anapofariki.

Lakini sasa madiwani wa mji huo wa Husavik wenye wakazi elfu 2, wameamua kusitisha utamaduni huo.
Wanasema utamaduni huo sasa haufai kwa sababu wakazi hawajuani kama ilivyokuwa zamani, na si lazima wakazi wawe wanamfahamu aliyefariki,hii ni kwa mujibu wa gazeti la Morgun bladid.
Mji wa Husavik huvutia sana watu wanaofika kutazama nyangumi,lakini diwani mmoja kutoka eneo hilo anasema kupeperushwa kwa bendera nusu mlingoti huwa kunashangaza watalii.
Uamuzi huo haukupitishwa kwa kauli moja na kumbukumbu za mkutano huo zilizopakiwa mtandaoni, zinaonyesha kuna madiwani kadha waliopinga mpango huo.
Mmoja wao Sofia Helgasdottir aliambia tovuti ya Visir kuwa, utamaduni huo ulianza zamani na wamekuwa nao, hivyo anafikiri ni utamaduni mzuri sana.

Kuhusu wageni kushangazwa amesema wageni hao ndio wanaofaa kujifunza tamaduni za wenyeji.

0 comments:

Post a Comment