Mahakama moja
nchini Ubelgiji, imeipa Facebook saa 48 kukoma kuwadukua watu ambao
hawajajiunga na mtandao huo wa kijamii.
Facebook imesema kuwa itakata rufaa uamuzi huo.
Kampuni hiyo ya mtandao wa kijamii inadai kuwa, mahakama hiyo
imetoa kauli hiyo kwa sababu ya programu ambayo imekuwa ikiitumia nchini humo
kwa kipindi cha miaka 5 sasa.
Programmu hiyo inajipachika kwa simu ya mtu aliyeingia kwenye
mtandao huo wa Facebook pale hata kama sio hajajiunga na mtandao huo wa
kijamii.
Hata hivyo mahakama hiyo Ubelgiji imesema kuwa Facebook haina
ruhusa ya kuwadakua watu ambao sio watumizi wa mtandao wake.
Na kama watataka kuwadukua, sharti wapate idhini ya mahakama.
Iwapo Facebook
itakataa kutii amri hiyo itatozwa faini ya Euro 250,000 kwa siku.
Programu hiyo aina ya Cookies inapigamsasa mtumiaji wa
Facebook ilikubaini kama yeye ama mashine anayoitumia imewahi kutumika kujiunga
na mtandao huo wa Facebook.
Msemaji wa Facebook alisema kuwa wamekuwa wakitumia programu
hiyo ya Datr kwa zaidi ya miaka 5 na hiyo ndio imekuwa ikisaidia kuhakikisha
akaunti za watu bilioni moja u nusu iko salama.
0 comments:
Post a Comment