Monday 9 November 2015

Kombe la dunia lilichangia mimba zaidi Afrika Kusini..!!!

Mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 2010 nchini Afrika Kusini, yalichochea ongezeko la idadi ya watoto wa kiume waliozaliwa nchini humo, miezi tisa baada ya mashindano hayo kuanza.

Hiyo ni kwa mjibu wa taarifa iliyochapishwa katika jarida la Early Human Development.
Kiwango cha wavulana waliozaliwa katika kipindi hicho kilikuwa kikubwa mno kati ya miaka 2003 na 2014.
Inasemekana kuwa kutokana na mchuano huo wa kombe la dunia, wanaume wengi walibaki makwao na hivyo kuchochea kufufuka kwa ndoa zilizokuwa zimefifia.

Watafiti hao wamesema kuwa watu walikuwa watulivu zaidi, na kuna uwezekano walijihusisha katika tendo la ndoa zaidi wakati wa mashindano hayo ya kombe la dunia, hali iliyofanya ongezeko kubwa ya idadi ya wanawake waliopata ujauzito.

0 comments:

Post a Comment