Benki
kuu ya Tanzania inasema kuwa imeipokonya leseni ya kuhudumu benki ya FBME ya
Tanzania baada ya kushutumiwa na serikali ya Marekani kwa utakatishaji wa fedha
haramu, kulingana na chombo cha habari cha Reuters.
Benki hiyo iliosajiliwa nchini
Tanzania ilikabiliana kisheria dhidi ya madai hayo ,lakini mahakama moja ya
Marekani ilitoa uamuzi uliopendelea idara ya fedha ya Marekani kwa kuchukua
hatua hiyo.
Kulingana na benki kuu ya
Tanzania mnamo tarehe 24 Julai 2014 Benki Kuu ya Tanzania iliiweka chini ya usimamizi
maalumu (statutory management) benki ya FBME Bank Limited (FBME).
Hatua hii ya Benki Kuu ilitokana
na Notisi iliyotolewa tarehe 15 Julai 2014 na Taasisi ya Marekani inayopambana
na Uhalifu wa Kifedha "the US Financial Crimes Enforcement Network"
kwa kifupi FinCEN, iliyoituhumu FBME kuwa ni taasisi inayojihusisha na biashara
ya utakatishaji wa fedha haramu
Uamuzi huo wa mahakama unaongeza
athari kwa kiwango kikubwa katika uendeshaji wa FBME kwa kuwa haitaweza tena
kufanya miamala ya kibenki ya kimataifa na kupata huduma za mifumo ya kibenki
na hivyo itashindwa kutoa huduma muhimu kwa wateja wake kwa mujibu wa leseni
waliyopewa.
Katika taarifa, benki kuu ilisema
kuwa imesitisha huduma zote za benki ya FBME na imeiweka chini ya ufilisi
Reuters inasema kuwa FBME
haikutoa mara moja tamko lake kuhusu hatua hiyo.
Benki ya FBME imesajiliwa katika
taifa hilo la Afrika mashariki lakini imekuwa ikitekeleza huduma zake katika
maeneo mengine hususan nchini Cyprus.
0 comments:
Post a Comment