Tuesday 9 May 2017

SIMBA WATANO WATOROKA MBUGA AFRIKA KUSINI.....

Polisi wakishirikiana na maafisa wa wanyamapori nchini Afrika Kusini wanawawinda simba watatu ambao wametoroka kutoka kwenye mbuga ya taifa ya Kruger.

Kutoroka kwa simba hao kumezua wasiwasi kwamba huenda wakawashambulia watu au mifugo.
Haijabainika ni vipi simba hao walifanikiwa kutoroka kutoka kwenye mbuga hiyo maarufu, lakini polisi wamewahimiza raia kuwa macho hasa katika maeneo yanayokaribia mpaka wa nchi hiyo na Msumbiji.
Msemaji wa polisi Leonard Hlathi alinukuliwa na eNCA akisema: "Wananchi wanafaa kuwa macho. Simba hao bado hawajakamatwa na wanasalia kuwa hatari kwa sababu barabara hiyo hutumiwa na watu wengi. Watu wanaopitia barabara hiyo wakiwa na magari wanaweza kuyaegesha kando ya barabara kwenda haja ndogo, jambo ambalo linaweza kuwaweka hatarini."
Taarifa ya Shirika la Mbuga za Taifa Afrika Kusini imesema wakazi wa eneo la Komatipoort na maeneo ya karibu katika jimbo la Mpumalanga ndio wanaofaa kutahadhari.
Msemaji wa shirika hilo Rey Thakhuli anaripotiwa kuwaona simba hao katika makutano ya barabara ya N4 / Mananga Jumatatu asubuhi eneo la Komatipoort.
"Inaaminika simba hao walitoweka na kuingia kwenye mashamba ya miwa kilomita nne kutoka kwa mbuga ya Kruger," amesema.
"Tunawahimiza watu wajiepushe kupiga picha wanyama hao watakapowaona kwani ni wanyama hatari…na inaaminika tayari wamemuua ng'ombe mmoja," amesema Thakhuli.
Mwaka uliopita, simba waliripotiwa kutoweka kutoka kwenye Mbuga ya Taifa ya Nairobi nchini Kenya na kuingia maeneo ya makazi.

Hakuna aliyeshambuliwa na wanyama hao.

0 comments:

Post a Comment