Takriban
watu 22 wamefariki baada ya ukuta kuwaangukia wakati wa harusi kaskazini mwa
India.
Wageni hao walikuwa wamejikinga
na mvua kubwa inayoendelea kunyesha kabla ya ukuta huo kuwaangukia.
Watu wengine 26 walijeruhiwa
katika jali hiyo ya Bharatpur,wilaya moja ya jimbo la Rajasthan , 15 kati yao
wakiwa na majeraha mabaya.
Vyombo vya habari vinasema kuwa
vibanda vya kuuza chakula vilikuwa vimewekwa kandakando ya ukuta huo karibu na
harusi.
Ukuta huo na kibanda ulianguka kutokana na kimbunga
kulingana na afisa wa Polisi Anil Tank aliyenukuliwa akisema.
Alisema kwamba ukuta huo wenye
urefu wa futi 90 uliwaangukia wageni wengi.
Waliojeruhiwa walikimbizwa katika
hospitali za eneo hilo mara moja huku wakipewa matibabu.
0 comments:
Post a Comment