Shule
zote katika kisiwa cha Zanzibar zimefungwa kwa muda kutokana na mvua kali
ambayo imesababisha mafuriko.
Waziri wa elimu katika kiswa
hicho Riziki Pembe Juma amesema kuwa mvua hiyo ambayo pia imekuwa ikinyesha
katika kisiwa cha Unguja na Pemba kwa kipindi cha wiki tatu zilizopita pia
imeharibu barabara na mali ya watu.
Alisema kuwa baadhi ya shule
zimejaa maji hivyobasi kuwa vigumu kwa walimu kufunza mbali na kuwa wanafunzi
wanashindwa kufika kutokana na mafuriko.
Waziri huyo amefichua kwamba uamuzi huo uliafikiwa
kufuatia pendekezo kutoka kwa kamati ya kukabiliana na majanga ya Zanzibar
ambayo iliishauri serikali kufunga shule hizo kwa usalama wa wanafunzi.
Baada ya kuangazia mapendekezo
hayo tulikuwa hatuna njia nyengine bali kuzifunga shule hadi pale hali
itakaporudia hali yake ya kawaida.
Hatahivyo amesema kuwa wanafunzi
wa kidato cha sita waliokuwa wakifanya mitihani yao ya mwisho wataendelea
kufanya hivyo.
Kufikia sasa kuna takriban
wanafunzi 364 495 wa shule za msingi na zile za upili zanzibar.
0 comments:
Post a Comment