This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Saturday, 7 March 2015

WAFANYAKAZI WA RADIO 5 WAPIGWA MSASA NA BBC MEDIA ACTION....

Wafanyakazi wa Radio 5 jijini A rusha wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kitaaluma ili

Wanawake wakulima wanaweza kutokomeza njaa

Wakati wa kuelekea siku ya wanawake duniani,viongozi wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani(FAO),Mfuko wa Kimataifa wa Kilimo na Maendeleo(IFAD)na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani(WFP) wamekutana mjini Roma,Italia ili kusisitiza jukumu la wanawake wakulima katika kufanikisha usalama na uhakika wa chakula. Kwa mujibu wa mashirika hayo matatu ya kimataifa,kuwezesha wanawake wakulima na kufikia usawa wa kijinsia kunachangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha usalama wa chakula na kupunguza umaskini vijijini. Akizungumza wakati wa mkutano huo mkuu wa IFAD Kanayo Nwanze,amesema nusu ya wakulima sasa ni wanawake wakati ambapo wanaume wanahamia mjini kutafuta riziki. Ameongeza kwamba ni lazima kutambua mchango wa wanawake ambao wanatekeleza kazi ngumu za kuvunja mgongo kwa ajili ya kulisha familia zao. Viongozi hao wamezingatia umuhimu wa kuwapatia wanawake fursa sawa za kufikisha bidhaa zao sokoni,kununua pembejeo na hatimaye kuwa na faida sawa kama wanaume.

Viapo vya ndoa havitekelezeki..!!!

Ahadi ya kuwa pamoja maishani katika shida na raha,taabu na shida viapo hivi ama ahadi hizi zinaonekana kuchukuliwa kirahisi mno na wanandoa wapya, lakini kwa muujibu wa utafiti mpya uliotolewa hivi karibuni unathibitisha kuwa ni rahisi mno kutamka kuliko utekelezaji wa viapo vyenyewe . Mtafiti uliofanywa kwa wanandoa wenye bahati 2,700 waliooana umegundua kwamba ,ikiwa mwanamke katika ndoa hiyo ataugua kwa muda mrefu asilimia sita hukaribia kupewa talaka kuliko wale ambao wana afya njema . Ukilinganaisha na wanaume ambao huugua wakiwa kwenye ndoa,hatari ya kuvunjika kwa ndoa ni ndogo mno,hatahivyo upendo huendelea hadi hapo mmoja wao atakapo baki kuwa mgane ama mjane. Utafiti ulioongozwa na wanazuoni wa chuo kikuu nchini Marekani,kinapendekeza kwamba kwa asili, wanawake wao wameumbwa kutoa huduma katika familia zao na hii inamaanisha kwamba wanaume wao huwa hawana uvumilivu wake zao pindi wanapokumbwa na maradhi ya muda mrefu ,ambayo pia yanweza kuwa hayatabiriki kuyakabili. Walifanyiwa utafiti wanandoa nchini Marekani,ambao wote walikuwa na umri wa miaka 50, mnamo mwaka 1990 ambao waliulizwa juu ya afya zao kuhusiana na maisha yao wakichnugza kwa miaka miwili,miwili ndani ya utafiti uliofanywa kwa miaka ishirini. Asilimia thelathini na mbili ya ndoa ziliishia kwa kuachana na asilimia ishirini na nnenzilivunjika kutokana na vifo vya mmoja wa wanandoa.

Friday, 6 March 2015

Ronaldo huijali mno Sanamu yake

Cristiano Ronaldo mara zote amekuwa na maamuzi ya kipekee yasiyo pitia kwa mtu wa pili na likija suala la kujijali ama kujipenda humwambii kitu hutekeleza ,suala ambalo limemfanya aonekane mchezaji wa kipekee mkubwa na imemjengea heshma kubwa. Lakini mkali huyu wa kabumbu anayesukuma gozi Real Madrid katika kujipenda amepiga hatua moja mbele yenye kuzua mjadala katika mitandao ya jamii na miongoni mwa watu wanaomfahamu ,na kama kinachosema na mtunza makumbusho wa timu Real Madrid ambaye kazi yake kubwa ni utunzaji wa sanamu za wachezaji na kuhakikisha hazipauki na kubaki kama wachezaji halisi walivyo . Gonzalo Presa, ndiye mhifadhi mkuu wa makumbusho hayo ya timu wa Real na ambaye pia ni mkurugenzi wa mawasiliano wa Museo de Cera ,ametema kwamba Ronaldo hutuma kinyozi wake binafsi mara moja kwa mwezi kuhakiki sanamu inayofanana naye iwe na muonekano anaoutaka. Na anasema kwamba Cristiano huwa anataka sanamu hiyo ichanwe nywele mara moja kwa mwezi,na nywele za sanamu hiyo zimeagizwa kutoka nchini India ni nywele halisi . Ronaldo mwenyewe ana makumbusho yake binafsi nchini Ureno,na makumbusho hayo yameendelea kuonesha mambo yamhusuyo tangu mwezi December,mwaka 2013.

Tamko la Facebook lamtia mashakani

Raia mmoja wa Marekani anayefanya kazi katika mataifa ya milki za kiarabu UAE, amekamatwa kwa matamshi aliyochapisha katika mtandao wake wa facebook na sasa anakabiliwa na hukumu ya kufungwa jela. Ryan Pate ambaye ni fundi wa ndege,alikuwa katika likizo ya kujiuguza nyumbani kwake katika jimbo la Florida nchini Marekani wakati alipomkosoa mwajiri wake. Aliita kampuni hiyo kama yenye ''wasaliti na kutoa matamshi ya kibaguzi dhidi ya watu wa mataifa ya milki hiyo. Wakati alipokuwa akirudi alikamatwa kwa kukiuka sheria kali za taifa hilo kuhusu matamshi ya kashfa. Iwapo atapatikana na hatia huenda akahudumia kifungo cha hadi miaka mitano jela.

Monday, 22 April 2013

Kwa nini binadamu hulia?Fahamu sasa..

 

 

 

Wanawake na wanaume hulia tofauti..

Watafiti wa  nchini Ujerumani walifanya utafiti kuhusu kulia na kubaini kuwa wanawake hulia kati ya mara 30 hadi 63 kwa mwaka na wanaume hulia mara 6 hadi 17 kwa mwaka.


Wanaume hulia kwa dakika mbili hadi nne wakati wanawake hulia kwa zaidi ya dakika sita.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Muhimbili, Dk Kitila Mkumbo anasema kitendo cha kulia kinatokana na mifumo ya hisia.
Anasema binadamu huweza kulia kutokana na hasira, maumivu au furaha.
Zipo aina tatu za machozi
Binadamu yeyote ana mirija ya machozi ambayo hutumika kulowanisha na kulinda macho yasiathiriwe na vumbi na vitu vingine.
Mirija hiyo ipo chini ya kope za juu na huzalisha maji yenye chumvichumvi ambayo ndiyo machozi-hayo  husambazwa katika jicho- kila  binadamu anapopepesa.
Wanasayansi wanasema, zipo aina tatu za machozi ambazo huzalishwa na macho ya binadamu.
Yapo machozi yajulikanayo kama ‘Basal’ au Basali. Machozi haya yana kazi kubwa ya kulinda jicho na kulipa unyevu.
Machozi mengine ni ya ‘Reflex’ haya yana kazi kubwa ya kutoa tahadhari kwa jicho pale linapoumia. Kwa mfano mtu akikata kitunguu au mdudu akiingia jichoni.
Machozi ya hisia au  ‘Pysch’ haya hutiririka pale ambapo binadamu hupatwa na uchungu, maumivu, msongo wa mawazo au furaha.
Tafiti zinaonyesha kuwa machozi ya hisia yana kiwango cha manganizi, chembechembe ambazo huathiri tabia au roho ya binadamu.
Machozi hayo ya hisia pia yana vichocheo vya prolactini ambavyo husimamia uzalishwaji wa maziwa.
Machozi yanayozalishwa kwa hisia yana mchanganyiko wa kemikali tofauti na aina nyingine za machozi.


Hivyo basi, binadamu anapolia, hutoa manganizi, potashiam na prolactini.
Chembechembe hizo zinatajwa kupunguza mshtuko au huzuni kwa  kuweka uwiano wa msongo wa mawazo katika mwili.

Sunday, 14 April 2013

Hatari:Aina Mpya ya Kisonono Yasambaa Duniani

ina mpya ya vimelea vya ugonjwa wa kisonono au "gono" ambavyo vinahimili dawa (resistant to drugs) zinazotumika kutibu ugojwa huu imegundulika duniani. Taarifa iliyotolewa na shirika la afya duniani (WHO) hivi karibuni imesema, ugonjwa wa kisonono unaoathiri mamilioni ya watu ulimwenguni umeanza kuwa sugu dhidhi ya dawa zinazotumiwa kuutibu na hivyo kuna hatari ya kutoweza kutibika kabisa.
Shirika la afya duniani limetoa wito kwa serikali na madaktari kuongeza ufuatlijiaji wa aina hii ya kisonono kutokana na ugonjwa wa kisonono kuwa na athari nyingi kama mcharuko (inflammation), ugumba, matatizo wakati wa ujauzito na hata vifo vya kina mama wajawazito.
“Aina hii mpya ya vimelea vya kisonono vinaonyesha usugu dhidhi ya dawa zote za antibiotiki tunazotumia dhidhi yake ikiwemo dawa za jamii ya cephalosporins ambazo ni dawa za mwisho katika kutibu ugonjwa wa kisonono, “ alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan, mmoja wa wanasayansi wa shirika la afya duniani katika kitengo cha magonjwa ya zinaa.
Miaka michache ijayo, aina hii mpya ya kisonono itakuwa sugu dhidhi ya dawa zote ambazo tunazo saizi “aliendelea kusema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan wakati wa mahojiano na shirika la habari la The Associated Press kabla WHO haijatangaza rasmi hatua na mwongozo mpya wa kukabiliana na tishio la aina hii mpya ya kisonono.
Inakisiwa watu milioni 106 ulimwenguni kote huathiriwa na ugonjwa wa kisonono kila mwaka.Ugonjwa wa kisonono pia huongeza hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa Virusi vya Ukimwi (VVU).
“Ugonjwa sugu wa kisonono sio tatizo la bara la Ulaya au Afrika pekee bali ni tatizo la dunia nzima kwa sasa,’” alinukuliwa akisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan.
Kwa mara ya kwanza, vimelea sugu vya ugonjwa wa kisonono dhidhi ya dawa aina ya cephalosporins  viliripotiwa katika nchi ya Japan, ikifuatiwa na Uingereza, Hongkong na Norway.
Wanasayansi wanaamini matumizi mabaya ya dawa aina ya antibiotiki pamoja na uwezo wa vimelea vya ugonjwa wa kisonono kubadilika na kuzoea mazingira mapya ndio chanzo kikuu cha kutokea kwa ugonjwa sugu wa kisonono na hivyo muda si mrefu ugonjwa huu utakuwa janga kubwa dunia nzima kama hatua za haraka hazitachukuliwa. Kuna uwezekano wa vimelea hivi sugu vya kisonono vinasambaa kwa sasa duniani bila kuweza kugundulika kutokana na nchi nyingi kutokuwa na ufuatiliaji na utunzaji kumbukumbu  mzuri wa wagonjwa wake.
Shirika la afya duniani limesema nchi zinatakiwa kuongeza ufuatiliaji wa wagonjwa wake pamoja na kudhibiti matumizi holela ya dawa za antibiotiki mpaka pale taarifa kamili za ugonjwa huu zitakapojulikana.
“Elimu ya masuala ya kujamiana pamoja na matumizi sahihi ya mipira ya kondomu inahitajika ili kutokomeza kabisa ugonjwa huu sugu wa kisonono. Hatuwezi kuutokomeza kabisa ugonjwa huu bali tunaweza kuzuia usambaaji wake,”alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan.

Protini Yagundulika Kusababisha Saratani ya Matiti kwa Wanawake Wanaotumia Vilevi

Kimengenyo (enzyme) ambacho ni protini aina ya CYP2E1 kimegundulika kuwa ndio chanzo kinachochangia wanawake kupata saratani ya matiti kwa wanawake wanaotumia vilevi. Kwa muda mrefu wanasayansi walikuwa wakitafuta uthibitisho wa uhusiano wa kunywa pombe na saratani ya matiti, lakini sasa wameweza kupata uhusiano huo. Protini hii hupatikana kwenye matiti ya wanawake na hivyo kuwaweka kwenye hatari kubwa ya kupata saratani ya matiti kama watakuwa wanakunywa sana vilevi kama pombe, whiskey, wine na nk.
Utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha Autonomous University of the State of Morelos cha nchini Mexico, umeonyesha ya kwamba protini hiyo ya aina ya CYP2E1 inauwezo wa kukivunja vunja kilewesho (ethanol) na kusababisha kutolewa kwa kemikali hatari zinazojulikana kama free radicals.
Watafiti hao wamesema ugunduzi wao utasaidia katika kuvumbua kipimo kitakachosaidia kujua ni wanawake gani walio na protini hii ya CYP2E1 na hivyo kuwasaidia kujikinga dhidhi ya saratani ya matiti.
Kemikali hizi hatari uhusishwa na kutokea kwa baadhi ya magonjwa kama saratani mbalimbali, ugonjwa wa kisukari, uharibifu wa mishipa ya damu aina ya ateri (arteries), kuchangia mtu kuzeeka na nk.
Swali kuu walilojiuliza watafiti wakati wa utafiti huo ni , Je kuwa na protini hii ya CYP2E1 kwa wingi huchangia mwanamke kupata ethanol-induced toxicity na hivyo kumhatarisha kupata saratani ya matiti?
Matokeo yetu yalionyesha ya kwamba seli za kutoka katika matiti ya mwanamke (mammary cells) zilizowekwa kilewesho cha aina ya ethanol, hutoa kemikali hatari kwa wingi, husababisha kuwepo kwa oxidative stress, huharakisha ufanyaji kazi wa seli na hivyo kuongeza kiwango cha ukuaji wa seli hizi kwa wingi na kusababisha saratani ya matiti” alisema Profesa Maria de Lourdes Rodriguez-Fragoso, kutoka chuo kikuu cha The Autonomous University of the State of Morelos cha nchini Mexico.
“Kama wewe ni mwanamke ambaye una kiwango kikubwa cha protini hii ya CYP2E1 katika matiti yako na unakunywa pombe basi utakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata saratani ya matiti ikilinganishwa na mwanamke ambaye ana kiwango kidogo cha protini hii katika matiti yake.” Aliendelea kusema Profesa Maria de Lourdes Rodriguez-Fragoso.
Uchunguzi uliofanywa kutoka kwenye tishu za matiti ya wanawake wenye afya njema ambao wamefanyiwa upasuaji wa kukuza matiti yao umeonyesha viwango tofauti vya protini hii katika wanawake hawa.
“Hii inamaanisha ya kwamba wanawake wanatafautiana kwa umengenywaji wa pombe na hivyo inabidi kila mwanamke kuchukua hatua tofauti katika kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya matiti” Alisema tena Profesa Maria de Lourdes Rodriguez-Fragoso.
Protini hii ya aina ya CYP2E1 hupatikana katika seli za matiti ya mwanamke zinazojulikana kama mammary epithelial cells ambapo pia ndio chanzo cha seli/chembechembe nyingi za saratani ya matiti na kusababisha watafiti hao kuanza kushuku uhusiano wake na saratani ya matiti.
Ili kuthibitisha shauku yao kwamba protini hii husababisha saratani ya matiti, watafiti hao walichukua tishu za matiti zilizo na viwango tofauti vya CYP2E1 na kuziweka kwenye pombe. Matokeo yalionyesha ya kwamba seli zenye kiwango kidogo cha protini aina ya CYP2E1 hazikuathiriwa sana ikilinganishwa na seli ambazo zilikuwa na kiwango kikubwa cha protini hiyo.
Utafiti huu ni ushindi mkubwa katika vita dhidhi ya saratani ya matiti kwani utasaidia kupunguza kiwango cha saratani hii kwa wanawake

Machungwa, Zabibu Hupunguza Uwezekano wa Kupata Kiharusi?

Utafiti mpya uliofanyika nchini Marekani  umesema ya kwamba kula machungwa na zabibu kunaweza kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi (Stroke).
Utafiti huo uliangalia faida za matunda chachu (Citrus Fruit) pekee kwa  mara ya kwanza tofauti na tafiti nyingi ambazo tumezizoea zinazoangalia umuhimu wa matunda na mboga za majani kwa afya kiujumla.
Utafiti huu umehusisha maelfu ya wanawake wanaoshiriki katika tafiti ya manesi  Nurse’s Health Study lakini wataalamu wanaamini faida hizo za machungwa na zabibu pia zinapatikana kwa wanaume.
 
Timu ya watafiti katika chuo cha Norwich Medical School katika Chuo Kikuu cha  East Anglia wamechunguza umuhimu wa kemikali aina ya flavonoids ambayo ni jamii ya antioxidant (kemikali zinauwa kemikali hatari za kwenye mwili) inayopatikana katika matunda, mboga za majani, chocolate nyeusi na wine nyekundu.
 
Utafiti huu ulifuatilia takwimu za miaka 14 za wanawake 69,222 ambao walikuwa wakishirki katika tafiti kwa kuandika kiwango chao cha kula matunda na mboga za majani kwa kila kipindi cha  miaka 4. Timu hiyo ya utafiti iliangalia uhusiano wa aina sita ya flavonoids - flavanones, anthocyanins, flavan-3-ols, flavonoid polymers, flavonols na flavones na hatari ya aina mbalimbali za kiharusi kama Ischaemic, Hemorrhagic na Total Stroke. Ilionekna wanawake waliokula kiwango kikubwa cha flavanones kwenye matunda chachu walikuwa na asilimia 19 ya uwezekano wa kupunguza kiharusi kulinganisha na wanawake ambao walikula kiwango kidogo cha matunda hayo.
 
Kiwango kikubwa cha flavanones kilikuwa 45mg kwa siku kulinganisha na kiwango kidogo cha  25mg kwa siku. Utafiti huu ulichapishwa katika jarida la Medical Journal Stroke umesema flavanones hupatikana kwa asilimia 82 kwenye machungwa na juisi ya machungwa na hupatikana kwa asilimia 14 kwenye zabibu na juisi ya zabibu.
 
Hata hivyo watafiti hao wamesema kwa wale wenye kusudio la kuongeza kiwango kikubwa cha flavanones itawalazimu kula tunda la chungwa kwa wingi na si juisi za machungwa zinazotengenezwa kiwandani kutokana na kiwango kikubwa cha sukari kinachopatikana katika juisi hizo za viwandani.
 
Professa Aedin Cassidy wa masuala ya lishe bora (nutrition) na ambaye alikuwa kiongozi wa utafiti huo amesema “kula kwa wingi kwa matunda, mboga za majani, na hasa Vitamin C uhusishwa na kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi”. Flavanones hutoa kinga dhidhi ya kiharusi kutokana na kuongeza ufanisi wa mishipa ya damu kwenye ubongo na kutokana na kuwa na uwezo wa kuzuia maambukizi mwilini (Anti-inflammatory effect).
 
Utafiti uliofanyika hapo awali ulionyesha ya kwamba ulaji wa matunda chachu na juisi yake na si matunda ya aina nyingine yoyote hupunguza uwezekano wa kupata  kiharusi aina ya Ischaemic Stroke na kuvuja damu kwenye ubongo (Intracerebral Haemorrhage).
 
 
Utafiti mwingine uliofanyika kipindi cha nyuma ulionyesha hakuna uhusiano wowote wa matunda ya njano na machungwa katika kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi lakini ulionyesha ya kwamba kuna uhusiano wa zabibu na mapeasi wa kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi.
 
Katika utafiti mwingine uliofanyika nchini Sweden umeonyesha ya kwamba wanawake ambao walikula  kiwango kikubwa cha antioxidant karibia asilimia 50 kutoka kwenye matunda na mboga za majani, ni wachache tu kati yao waliopata kiharusi ikilinganishwa na wanawake ambao walikuwa na kiwango kidogo cha antioxidant.
 
Matokeo ya utafiti huu yasiwafanye watu kuacha kula matunda ya aina nyingine pamoja na mboga za majani kwani nayo yana faida kubwa katika mwili wa binadamu.
 
Kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi inawezekana kama mtu atakula lishe bora iliyo na virutubisho vyote muhimu, kula matunda na mboga za majani kwa wingi, kufanya mazoezi mara kwa mara, kupunguza kiwango cha ulaji chumvi (kwani watu wenye asili ya Kiafrika wana kiashiria cha asili kinachojulikana kama salt retention gene ambacho hufanya kiwango kidogo cha matumizi ya chumvi mwilini kuonekana kama kiwango kikubwa na hivyo kuongeza hatari ya kupata kiharusi),kupunguza uzito (kuwa kwenye uzito unaotakikana kiafya  kulingana na umri na urefu wako), kupunguza kiwango cha matumizi ya mafuta katika chakula, kulala masaa ya  kutosha na kupunguza msongo wa mawazo. 


Friday, 12 April 2013

Upara,sababu ya maradhi ya moyo?....



Wanaume wanaoanza kuwa na upara huenda wakakabiliwa zaidi na tisho la maradhi ya moyo kuliko wenzao waliojaa nywele vichwani.
Hii ni kwa mujibu wa watafiti nchini Japan.
Utafiti huu uliowahusisha watu elfu 37,000, ulichapisha taarifa kwenye jarida la mtandao, 'BMJ Open' ukisema kuwa wanaume wanaokuwa na upara kwa asilimia 32 wanaweza kuwa na maradhi ya moyo.

Hata hivyo watatifi walisisitiza kuwa athari hizi ni chache ikilinganishwa na zile za uvutaji sigara na unene kupita kiasi.

Shirika linalojikita katika maswala ya maradhi ya moyo nchini Uingereza, limesema kuwa wanaume wanapaswa kujichunga wasinenepe kupita kiasi kuliko kuchunga nywele zao.

Kuanza kukuwa na kipara ni kawaida ya maisha kwa wanaume .

Wengi kuanza kukuwa na upara wanapokuwa miaka 50 na asilimia 80 ya wanaume hao, hupoteza nywele wanapokuwa na umri wa miaka 70.

Watafiti katika chuo kikuu cha Tokyo, walidurusu utafiti wa miaka mingi iliyopita, kuchunguza uhusiano uliopo kati ya kuwa na upara na maradhi ya moyo.

Walionyesha kuwa nywele ambazo zilianza kutoweka, zina uhusiano na maradhi ya moyo.

Hii ilikuwa baada ya kuzingatia maswala kama umri, na historia ya familia.

Daktari Tomohide Yamada wa chuo kikuu cha Tokyo,amesema kuwa walipata uhusiano mkubwa kati ya upara na tisho la kupata maradhi ya moyo.

Amesema kuwa wanaume wenye umri mdogo wanaopata upara wanapaswa kuanza kuzingatia afya njema ili kujikinga kutokana na maradhi ya moyo

Aidha amesema hakuna ushahidi wa kutosha kupendekeza kuwa wanaume wenye upara wafanyiwe uchunguzi wa maradhi ya moyo.

Maradhi ya moyo ndio moja ya sababu kuu za vifo nchini Uingereza.

Mmoja kati yawanawake wanane kufariki kutokana na maradhi ya moyo.

Husababishwa na mishipa ya damu ambayo husukuma damu kwa moyo pale inapoziba.

Mmoja wa madaktari wakuu Uingereza amesema kuwa ingawa utafiti huu unaibua hisia, wanaume wenye upara hawapaswi kuwa na hofu.

Wednesday, 27 February 2013

Hivi ni vivutio vya Tanzania vilivyoingia katika maajabu saba ya asili Afrika. Serengeti Migration, Mlima Kilimanjaro na Ngorongoro crater.

Ni Katika kile kinyang'anyiro cha kupata vivutio asilia saba vyenye maajabu toka barani Afrika. Kinyang'anyiro ambacho kilirindima mwaka jana 2012 kwa wadau kupigia kura vivutio 11 vilivyokuwa vikishindanishwa. Mlima Kilimanjaro,Wanyama wanaohama wa Serengeti na Ngorongoro crater ndio yalikuwa maajabu toka Tanzania ambayo yalikuwa yameteuliwa kupigiwa kura,kwa kifupi vivutio vyote vitatu toka Tanzania vimeweza kufanya vyema. Taarifa ya vivutio vitatu kutoka Tanzania kuingia kwenye orodha ya vivutio 7 vya ajabu barani Afrika iliwekwa wazi mjini Arusha,ambako kulikuwa na sherehe rasmi ya kuvitaja vivutio vilivyoingia kwenye orodha hii baada ya zoezi la kupiga kura kusitishwa mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka 2012. Katika hafla hiyo,Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ndio alikuwa mgeni rasmi. Matokeo hayo yalitangazwa na Dk,Phillip Imler ambaye ni rais wa taasisi ya Seven Natural wonders of the world. Vivutio vingine viliweza kuingia kwenye orodha hii ni Okavango Delta, Red Sea Reef, Jangwa la Sahara na Mto Nile. Tanzania ndio nchi pekee iliyoweza kuingiza vivutio 3 kwenye orodha hii kwa mwaka 2012. Kiwale11 Bloga inatoa pongezi kwa wote waliotikia wito na kupiga kura na kuiwezesha nchi yetu kutoka kifua mbele kwa kuingiza vivutio 3 kwenye orodha hii.

Mazoezi makali yanaongezea umri?..

Wewe ni mkimbiaji au muinua vyuma? Wakimbia katika mbio za masafa marefu au katika mashindano ya michezo mitatu tofauti - triathlon? Ni mazoezi yapi ambayo unaweza kufanya ikiwa unataka kujiongezea umri? Je, ni vyema zaidi kufanya mazoezi mafupi na makali, au marefu zaidi lakini ya taratibu? Kwa mujibu wa Daktari Jamie Timmons, Profesa wa masomo ya bayologia ya uzee katika Chuo Kikuu cha Birmingham, dakika tatu za mazoezi makali kila juma kwa majuma manne kunaweza kukaboresha, kwa kiwango kikubwa, afya ya mtu. Mazoezi haya makali yanaweza kusaidia moyo na mapafu yako kusambaza hewa mwilini vyema zaidi. Pia yanaboresha ifanyavyokazi insulini, ambayo inaondoa sukari mwilini na kudhibiti mafuta. Nao utafiti wa Daktari Stuart Gray wa Chuo Kikuu cha Aberdeen unadhihirisha kwamba mazoezi makali na mafupi, kama kukimbia kwa kasi kwa masafa mafupi, au kuendesha baiskeli kwa sekunde 30 tu, kunaufanya mwili uondoe mafuta kutoka kwenye damu haraka zaidi kuliko kufanya mazoezi ya wastani, kama kutembea harakaharaka. Kuondolewa kwa mafuta kutoka kwenye damu ni muhimu kwa vile kunapunguza uwezekano wa kukumbwa na tukio la mshtuko wa moyo.

WABUNGE WAZICHAPA WAKATI WA MDAHALO KWENYE TV.SHOW

a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvUE-3IdrVzVDdRAkVbf9UX_oBv3ikVHMaFcJI1Y3xPsFr_S-9GkT88Na1XAkSmD_3ueR2QJbG30bDAu7srtfgqdHUhYVAVmDz59yOUyI-nEgLEKJGZgtFUO6Q-_ipPrX4GghyROySGXX3/s1600/wabunge.jpg" imageanchor="1" > Wabunge wawili wapigana makonde wakati wa kipindi cha mdahalo kwene runinga ya kitaifa huku Georgia. Huko Lebanon wabunge wengine wawili pia warushiana glasi za maji na baadae kupigana ngumi vilevile wakati wa mdahalo kwenye Televisheni. Hii ni baada ya wabunge hao kuhitalafiana kuhusu vita vinavyoendelea nchini Syria baina ya waasi na serikali ya Rais Basher al Assad.

Monday, 17 December 2012

Fahamu Siri ya herufi ya mwanzo ya Jina lako...

Je Unajua Siri ya herufi ya mwanzo ya jina lako?. Soma hapa utaweza kuelewa Tabia zako au tabia za rafiki au mpenzi wako. >HERUFI A >Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. Herufi A inawakilisha Nyota ya Punda. >HERUFI B >Mwenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. Herufi B inawakilisha Nyota ya Ngombe, >HERUFI C >Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano Herufi C inawakilisha Nyota ya Mapacha, >HERUFI D >Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. Herufi C inawakilisha Nyota ya Kaa, >HERUFI E >Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. Herufi E inawakilisha Nyota ya Simba, > >HERUFI F >Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. Herufi F inawakilisha Nyota ya Mashuke, >HERUFI G >Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu. Herufi G inawakilisha Nyota ya Mizani, >HERUFI H >Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. Herufi H inawakilisha Nyota ya Nge, >HERUFI I >Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. Herufi I inawakilisha Nyota ya Mshale, >HERUFI J >Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. Herufi J inawakilisha Nyota ya Mbuzi, >HERUFI K >Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. Herufi K inawakilisha Nyota ya Ndoo, >HERUFI L >Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. Herufi L inawakilisha Nyota ya Samaki, >HERUFI M >Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda >HERUFI N >Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. Herufi N inawakilisha Nyota ya Ngombe > >HERUFI O >Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia. Herufi O inawakilisha Nyota ya Mapacha >HERUFI P >Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi P inawakilisha Nyota ya Kaa >HERUFI Q >Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana. Herufi Q inawakilisha Nyota ya Simba >HERUFI R >Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani. Herufi R inawakilisha Nyota ya Mashuke >HERUFI S >Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi S inawakilisha Nyota ya Mizani >HERUFI T >Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika. Herufi S inawakilisha Nyota ya Nge >HERUFI U >Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mshale. >HERUFI V >Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mbuzi. >HERUFI W >Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari. Herufi W inawakilisha Nyota ya Ndoo. >HERUFI X >Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi X inawakilisha Nyota ya Samaki. >HERUFI Y (YASINTA) >Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha. Herufi Y inawakilisha Nyota ya Punda >HERUFI Z >Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ngombe.

Wednesday, 12 December 2012

UNAJUA KUWA SHULE YA KWANZA TANZANIA ILIJENGWA MUHEZA TANGA?

HAYA NI BAADHI YA MAJENGO YALIYOJENGWA KATIKA SHULE HIYO BAADAE.... MWAKA 1848 Mmishenari wa Kijerumani Dk Johan Ludwig Krapf,alitembelea kijiji cha Magila kilichopo Muheza mkoani Tanga akiwa katika safari zake za Afrika Mashariki. Magila kuna mlima ulio katika safu za milima ya Usambara ukipakana na mlima wa Magoroto ambao ndio chanzo cha maji ya mto Mkurumuzi unaoelekea Muheza. Historia inaonyesha eneo la mlima Magila wenye miamba na mawe mengi, zamani kabla ya kuja wageni lilitumika kuwatenga wagonjwa wa ukoma na magonjwa mengine yasiyotibika, kwa lengo la kuwazuia wasiwaambukize wengine. Dk Krapf alipofika na kuwaona wagonjwa hao waliokuwa wakiishi kwa madhila makubwa, alichonga msalaba katika mti wa mkuyu kwa imani kuwa Mwenyezi Mungu angewaponya wagonjwa hao. Eneo hilo ndilo lililokuja kujengwa shule ya kwanza na Waingereza mwaka 1886. Alama ya msalaba huo ipo hadi na sasa na ndipo ilipo Shule ya Sekondari Hegongo. Hadi leo mahali hapo panaitwa Magila Msalabani. Kwa sasa Magila ni kata yenye vijiji vya vya Magila, Mikwamba, Misongeni na Mafleta. Mkaazi wa eneo hilo Luteni Kanali mstaafu John Mhina amekamilisha kuandika kitabu kuhusu historia ya Magila Msalabani,kinachoeleza historia ya kijiji hicho na ujio wa wazungu walioanzisha shule ya kwanza Tanganyika na kanisa. Luteni Kanali Mhina aliyelitumikia Taifa kwa muda mrefu kama mwanajeshi, na baadaye kuwa Mbunge wa Muheza kutoka mwaka 1990 hadi 1995,anasema harakati za kuanzisha shule katika kijiji hicho zilitokana na Wamishenari waliokuja Afrika Mashariki kutoka Ulaya kwaajili ya kueneza dini ya kikristo tangu miaka ya 1770. Anawataja baadhi ya Wamishenari hao kuwa ni pamoja na David Livingstone,Charles Mackenzie, William Tozer na Edward Steer. Anasema harakati hizo zilianzia tangu visiwa vya Zanzibar mwaka 1863 ambako pia walikomesha biashara ya utumwa na kuanza ujenzi wa kanisa la Anglikana la Mkunazini Zanzibar kwa miaka 10 tangu mwaka 1873. Anasema wakati huo kulikuwa na shule iliyoanzishwa Zanzibar maeneo ya Kiungani na Kiinua mguu na Askofu William Tozer mwaka 1869. Hata hivyo, anasema shule hiyo haikuwa rasmi na ilikuwa ikifundisha elimu ya dini kwa watumwa waliokombolewa.