Wednesday 23 September 2015

Dawa ya kupunguza makali ya HIV yapanda kwa 5000%...

Kampuni moja ya kutengeza madawa imelazimika kujitetea vikali baada ya kupandisha gharama ya dawa ya kupunguza makali ya Ukimwi kwa asilimia elfu 5.

Hii inamaanisha kuwa bei ya tembe moja ya dawa inayotumika kupunguza makali ya ukimwi itapanda kutoka dola $13.50 hadi $750.
Kampuni hiyo inayoitwa Turing Pharmaceuticals, imelaumiwa na washika dau wa maswala ya Ukimwi kwa kuongeza bei ya dawa hiyo ya Daraprim, ambayo imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha uwezo wa mwili wa mgonjwa aliyeathirika kupigana na maambukizi mapya.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Martin Shkreli, amenukuliwa akisema kuwa faida itakapatikana baada ya mauzo ya dawa hiyo, itasaidia kugharamia utafiti wa dawa mpya na zenye ubora zaidi.
Tembe moja ya dawa hiyo ya Daraprim inagharimu dola moja pekee kuitengeneza.
Hata hivyo bwana Martin anasema kuwa bei hiyo haijumuishi gharama ya kunadi dawa hiyo wala usambazaji wake, ingawa gharama imeimarika maradufu katika miaka ya hivi punde.
Daktari Wendy Armstrong kutoka muungano wa wauguzi nchini Marekani HIV Medicine Association, amekashifu sababu zilizotolewa kwaajili ya nyongeza hiyo kubwa ya bei ya dawa hiyo.

Katika siku za hivi karibuni dawa za kupunguza makali ya saratani, zinagharimu dola laki moja ilhali gharama yake asili inaweza kugharimu dola nusu milioni.

0 comments:

Post a Comment