Monday 21 September 2015

Mali ya serikali ya Zimbabwe yapigwa mnada.

Nyumba inayomilikiwa na serikali ya Zimbabwe imeuzwa $280,000 (£180,000) kupitia mnada Afrika Kusini.

Mwekezaji katika nyumba Arthur simatakopoulos amenunua nyumba hiyo iliyoko mji wa Cape Town, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Mohammed Allie.
Mnada huyo umefanyika baada ya serikali hiyo kushindwa kwenye vuta nikuvute iliyodumu miaka mitano na shirika la kutetea haki za Waafrikaner nchini Afrika Kusini kwa jina AfriForum.
Shirika hilo liliitaka serikali ya Zimbabwe kulipa gharama ya kesi baada ya serikali hiyo kushindwa kwenye kesi iliyohusu mageuzi ya umiliki wa mashamba.
Serikali ya Zimbabwe chini ya Rais Robert Mugabe ilikuwa imechukua mashamba kutoka kwa Wazungu na kuyapa Waafrika weusi.
Mahakama maalum ya muungano wa mataifa ya Afrika Kusini (Sadc) iliamua 2008 kwamba mpango huo ulikuwa kinyume cha sheria, shirika hilo lilisema.
Mahakama Kuu mjini Pretoria iliwaagiza maafisa nchini Afrika Kusini kutwaa mali hiyo 2010.
Zimbabwe ilifika kortini mara kadha kupinga uamuzi huo bila mafanikio.


0 comments:

Post a Comment