Tuesday 29 September 2015

Maji yagundulika katika sayari Mars…………

Wanasayansi wametangaza kuwa kuna ushahidi wa kuaminika kuwa,kuna maji katika sayari ya Mars na hivyo kuibua matumaini kuwa kuna uwezekano wa viumbe kuishi katika sayari hiyo.

Wataalamu kutoka taasisi ya utafiti wa safari za anga ya juu ya Marekani NASA, wamesifu ugunduzi huo wa wanasayansi na kusema kuwa, unatoa ufahamu zaidi kuhusu sayari ya karibu na dunia kuwa sio kavu kama ilivyodhaniwa hapo awali.

Mkurugenzi wa NASA Jim Green, amewaambia wanahabari mjini Washington Marekani kuwa, kugundulika kwa maji katika sayari ya Mars ni habari njema kuwa viumbe hai vinaweza kuishi katika sayari hiyo. 

0 comments:

Post a Comment