Thursday 29 June 2017

HELIKOPTA ILIYOTUMIKA KUSHAMBULIA MAHAKAMA YAPATIKANA VENEZUELA…..

Vikosi vya usalama nchini Venezuela vimepata helikopta iliyotumiwa na afisa muasi wa polisi kupaa juu ya majumba ya serikali mjini Caracas huku ikikiangusha guruneti na kupiga risasi siku ya
Jumanne.

Makamu wa rais wa Venezuela, Tareck El Aissami, amesema helikopta hiyo ilipatikana karibu na karibu na jimbo la Vagas pwani kaskazini, kilo mita arubaini na tano kutoka mji mkuu wa Caracas.
Aliatoa picha zinzo inayoonyesha helikopta hiyo katika maeneo ya milima ikisafisha maeneo yaliyozungukwa na migomba ya ndizi.
Kufikia sasa hakuna dalili yakupatika na kwa rubani Oscar Lopez, afisa huyo wa polisi huku serikali ikitaja kisa hicho kuwa kitendo cha ugaidi.

0 comments:

Post a Comment