Tuesday 20 June 2017

WANASAYANSI KUJA NA TIBA MBADALA YA MAGONJWA YA MOYO….

Wanasayansi nchini Nethelands wameanza kufanya majaribio ya chanjo ya kupunguza kiwango cha mafuta mwilini mwa binadamu ambapo kama itafanikiwa kuna matumaini makubwa ya
kupunguza magonjwa ya moyo.
Watafiti hao wamesema kuwa majaribio yao waliyokwisha kuyafanya dhidi ya panya yanaonesha kwamba chanjo hiyo imefanikiwa kuzuia na kuacha kuimarisha amana ya mafuta katika mishipa ya damu
Wamesema kuwa chanjo hiyo inaweza kutumika kama njia mbadala ya kupunguza na kuwasaidia mamilioni ya watu ulimwenguni kupambana na mafuta yasiyohitajika mwilini hivyo kupunguza magonjwa ya moyo.

Hata hivyo, chanjo hiyo inatarajiwa kuchukua takribani miaka sita ili vipimo hivyo kuanza kufanya kazi kwa binadamu kwa kutoa tiba ambayo itakuwa ni mkombozi kwa wagonjwa.

0 comments:

Post a Comment