Tuesday 20 June 2017

MBARONI AKIPENYEZA SIMU TANO GEREZA LA KEKO DAR…

Ramadhani Nombo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Chang’ombe Temeke jijini Dar es Salaam, kwa kosa la kupenyeza simu tano kwenye gereza la Keko.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya chakula alichopeleka gerezani, kutoa mlio wakati wa ukaguzi.
Kitendo hicho kilitiliwa shaka na askari magereza ambao walikikagua.
Walipochunguza zaidi waligundua kuwa kwenye chakula hicho, kulikuwa na simu tano.
Nombo aliweka simu hizo tano zikiwa zimezungushiwa karatasi ya plastiki nyepesi kuzuia uharibifu, na kuweka katikati ya chakula aina ya ndizi nyama, ambazo zilikuwa kwenye bakuli kubwa.
Lakini zoezi hilo halikuweza kufanikiwa baada ya kubainika na kutiwa nguvuni.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam Augustine Mboje, alisema mtuhumiwa anashikiliwa Kituo cha Polisi Chang’ombe na baada ya mahojiano kwa kina atapandishwa kizimbani, kwani kitendo alichofanya ni uhalifu kama ulivyo uhalifu mwingine.

0 comments:

Post a Comment