Friday 22 July 2016

2016 WAELEKEA KUWA MWAKA WENYE JOTO KALI KUWAHI KUREKODIWA..!

Mwaka huu wa 2016 huenda ukawa ndio wenye joto kali zaidi kuwahi kurekodiwa, kufuatia hali ya joto
duniani kuweka rekodi mpya ya viwango vya nyuzi joto katika miezi sita ya kwanza.
Hayo ni kwa mujibu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), ambalo limesema barafu ya bahari ya Arctic iliyeyuka mapema na kwa kasi, ambayo ni ishara nyingine ya mabadiliko ya tabianchi.
Aidha shirika hilo limesema kuwa viwango vya gesi ya mkaa, ambavyo vinachangia ongezeko la joto duniani, vilifikia upeo mpya.


Katibu Mkuu wa WMO Petteri Taalas amesema kuwa, hali ya El Nino ya 2015/2016 imechangia viwango hivi vya joto.

0 comments:

Post a Comment