Friday 22 July 2016

PANYA SASA KUTUMIA UZAZI WA MPANGO…!

Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), kimepata suluhisho la kupunguza kuzaliana panya nchini kwa

kuanzisha uzazi wa mpango kwa wanyama hao.

Akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam Mtaalamu wa Kilimo wa Chuo hicho Thoneson Mhamphi, amesema utafiti huo ambao upo katika hatua za awali haujaweza kusambazwa.
Mhamphi amesema dawa hizo za uzazi wa mpango zinazojulikana kama Quinestro na Levonorgester, zimekuwa zikichanganywa kwenye chakula na kuwapatia panya hao hatua itayowafanya washindwe kuzaliana.
Amesema utafiti huo unaendelea kufanyika katika hatua nyingine, kuona jinsi ya kukabiliana na panya waliopo mashambani.
Msikilizaji kama hukuwa ukifaamu ni kwamba, panya wana kasi ya kuzaliana na anaweza kuzaa kila baada ya wiki tatu.

Vilevile panya ana uwezo wa kupata mimba tena saa 24 baada ya kuzaa.

0 comments:

Post a Comment