Thursday 28 July 2016

TANZANIA KINARA WA SOKO LA SIMU AFRIKA…

Ripoti ya mwaka 2016 ya Uchumi wa Simu za Mikononi Afrika inasema kuwa,

Tanzania ni miongoni mwa nchi nane Afrika zenye soko kubwa la simu za mikononi.

Ripoti hiyo iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana kwenye mkutano wa wanne wa mwaka wa Chama cha Kampuni za Simu (GSMA Mobile 360 Afrika), inatokana na utafiti uliofanywa na GSMA Afrika.
Ripoti hiyo inasema Tanzania inaungana na nchi za Nigeria na Ethiopia ambazo kwa utatu wao, ndio zinazochukua zaidi ya theluthi moja ya soko simu ya mikononi barani Afrika.

Ripoti hiyo imebainisha kuwa zaidi ya watu nusu bilioni Afrika wamejiunga na huduma ya simu za mkononi, na wengi wao wakijiunga na huduma na intaneti inayopatikana kwenye simu zao.

0 comments:

Post a Comment