Monday 4 July 2016

MAJAJI WAJINOA MAHAKAMA YA UFISADI…!!

Jaji Mkuu wa tanzania Mohamed Chande amesema kuwa, jopo la majaji linatarajiwa kuingia darasani ili


kujifunza sheria mpya ya kuendesha kesi za ufisadi.

 Kesi hizo zitakuwa zinaendeshwa katika Mahakama Kuu Kitengo cha Uhujumu Uchumi, na tayari majaji 14 wa wataanza kozi maalumu ya siku tano katika Chuo cha Sheria kilichopo Lushoto, Tanga.
 Amesema hatua hiyo inakuja baada ya wiki iliyopita, Bunge kupitisha sheria ya uhujumu uchumi ya mwaka 2002 ikiwa na maboresho mbalimbali.

Ameongeza kuwa maeneo yapo tayari na wameshapeleka wasajili na watendaji ambao wameanza kufanya kazi,na baada ya michakato mingine kukamilika kila kitu kitakuwa sawa na majaji wataanza kazi.

0 comments:

Post a Comment