Thursday 14 July 2016

UTAFITI:UNENE UNAUA MAPEMA…!!

 
Utafiti wa kimataifa umegundua kuwa kunenepa kunahusiana moja kwa moja na visa vya watu kufa
mapema, huku wanaume wakiwa katika uwezekano mara tatu wa kufariki zaidi ya wanawake.

Kwa kutumia data kutoka takriban watu milioni 4 kutoka mabara manne, Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Lancet unaashiria kwamba watu wanene wanakufa kwa kiasi cha miaka mitatu mapema tofauti na watu walio na unene wa kawaida.
Watu walio na unene wa kupindukia wanapoteza miaka kumi ya maisha yao ambayo wangeweza kuishi.
Wanasayansi wanasema kwamba kuwa na uzito mkubwa wa mwili kunaongeza hatari ya kuugua maradhi ya moyo na ya mapafu, kiharusi na saratani.
Utafiti huo mpya unatofautiana na matokeo ya utafiti wa awali yaliyoashiria kwamba kuwa mnene kuna manufaa ya kuishi zaidi.

Badala yake watafiti wanasema moja kati ya vifo vitano vya mapema Marekani na moja kati ya vifo 7 vya mapema Ulaya, vinatokana na kunenepa kupindukia.

0 comments:

Post a Comment