Tuesday 5 July 2016

WAZIRI MKUU APIGA MARUFUKU SHISHA NCHI NZIMA,HAYA HAPA MADHARA YAKE..!

Waziri mkuu Kassim Majaliwa, amepiga marufuku uvutaji wa shisha nchini, na kulitaka Jeshi la
Polisi kufuatilia na kutokomeza matumizi ya sigara hiyo ili kuokoa makundi ya vijana ambao wanajihusisha na ulevi huo.
Waziri mkuu Majaliwa alitoa agizo hilo juzi jijini Dar es Salaam katika futari iliyoandaliwa na waumini wa dini ya kiislamu wa madhehebu ya Shia.
Amesema shisha inamchanganyiko mwingi na wanaweza kutia maji, lakini wakati mwingine maji hayo yakawa yamewekwa gongo na vilevi vingine mbalimbali.
Waziri mkuu Majaliwa alisema mtu anapotumia kilevi hicho anakuwa anashawishika kila siku kukitumia, na kwamba pale anapokikosa husikia mwili unasisimka na hivyo kulazimika kuifuata popote pale ilipo.
Juzi akizungumza jijini Dar es Salaam Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda, alipiga marufuku uvutaji wa sigara hadharani, pamoja na matumizi ya sigara ya shisha mkoani humo kwa kuwa inachanganywa na vilevi vinavyoharibu vijana.
Alisema utafiti alioufanya chini ya Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), shisha ina madhara makubwa kwa wanaoivuta na wasiovuta kwa kusababisha saratani ya mapafu na koo.
Msikilizaji kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kiwango cha shisha inayovutwa kwa saa moja, ni sawa na kuvuta sigara kati ya 100 na 200.
Msikie hapa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda,akizieleza adhari anazoweza kuzipata mtumiaji wa shisha.

0 comments:

Post a Comment