Monday 4 July 2016

SOKO LA PANYA WA SUA LAONGEZEKA…!

Soko la panya waliogunduliwa na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) wenye uwezo wa kutegua
mabomu na kubaini ugonjwa wa kifua kikuu, limezidi kuongezeka baada ya nchi nyingi kuwahitaji.

Nchi za Cambodia, Vietnam, Thailand na nyinginezo zilizopitia katika vita, zimeonesha kufanikiwa na panya hao, na sasa wanahitaji wengine zaidi ya 10 ili kusambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi hizo.
Pia nchini Ethiopia wamehitaji panya zaidi ya 10 kwa ajili ya kubaini ugonjwa wa kifua kikuu, kutokana na panya hao kuwa na uwezo wa kubaini mgonjwa ambaye ugonjwa huo haujaonekana kwa vipimo vya kawaida.
Mtafiti wa Kituo cha Utafiti na Udhibiti wa Viumbe Hai Waharibifu wa SUA Dk Georgies Mgode,amesema awali panya wa kutegua mabomu waliishapelekwa katika nchi za Msumbiji, Angola na 16 Cambodia na kuonesha mafanikio makubwa sana.

Amesema kwa sasa wanaomba vibali katika Wizara ya Maliasili na Utalii kupeleka panya hao wanaohitajika, katika mwisho wa mwaka huu au mwanzoni mwa mwakani.

0 comments:

Post a Comment