Waumini
wanawake wanaokwenda kufunga ndoa katika Kanisa Katoliki Parokia ya
Hananasif
Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamepigwa marufuku kupaka rangi ya
mdomo Lipstick’ wakati wa ibada ya misa takatifu ya ndoa.
Rangi hiyo ya mdomo ni moja ya vipodozi ambavyo
hutumiwa na wanawake kwa ajili ya urembo, kwa lengo la kunogesha mwonekano wake
na kuvutia mbele za watu.
Uamuzi huo ulitangazwa juzi jioni na Paroko wa Parokia
ya Hananasif Kinondoni jijini Dar es Salaam Padri Gasper Mtengeti, wakati wa
ibada ya misa ya kumwombea marehemu Rose Michael iliyofanyika kanisani hapo.
Kutokana na hali hiyo Pandri Mtengeti amewataka
wanawake kuacha kupaka rangi wakati wa misa takatifu, ambapo alitoa sababu
tatu zinazotokana na Liturijia ya Ekaristi Takatifu (utaratibu wa uendeshaji wa
ibada) chini ya Kanisa Katoliki.
Pandri Mtengeti ameeleza sababu hizo kuwakataza
maharusi wa kike kujipaka rangi ya mdomo, ambapo amesema rangi hiyo inayopakwa
huwa inasalia katika chombo kinachobeba divai ambayo kiimani kwa dhehebu hilo
ni Damu ya Yesu Kristu.
Sababu
ya pili ni kwamba rangi ya mdomo huwa inachanganyika na damu ya Yesu wakati
wanapokunywa, kitendo ambacho si chema mbele za Mungu.
Na sababu ya tatu rangi hizo hubaki kwenye kitambaa
cheupe, kinachotumika kufuta kikombe cha hostia baada ya kuguswa na midomo ya
mtu mara baada ya kunywa.
0 comments:
Post a Comment