Raia wa China wameelezwa kuongoza kuingia nchini kinyume cha sheria,
katika kipindi cha
miezi minne (Januari mpaka Aprili) wakifuatiwa na
Waethiopia.
Naibu Kamishna wa Uhamiaji Divisheni
ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Wilson Bambaganya, ametoa taarifa hiyo jana
katika mkutano na wanahabari akisema jumla ya wahamiaji haramu elfu 4 mia 7 na 92
wamekamatwa nchini katika kipindi hicho.
Amesema changamoto kubwa katika
udhibiti wa wahamiaji haramu ni ukubwa, na uwazi wa mipaka yetu sanjari na
uwanda mkubwa wa bahari.
Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Utawala
na Fedha ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Abbas Irovya, amesema
operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu nchini imefanikisha kubaini
waliokamtwa.
0 comments:
Post a Comment