Waziri
mkuu wa Uingereza, David Cameron, ametangaza atajiuzulu, baada ya kushindwa
kuwashawishi raia wengi wa Uingereza, kusalia katika muungano wa Ulaya.
Cameron akiwa amejawa na huzuni
amesema kuwa atasalia ofisini kwa siku tisini zijayo ndipo angatuke.
Bw Cameron ambaye ameongoza
kampeini ya kusalia katika muungano wa EU amesema kauli hiyo imempa mshutuko
mkubwa na kwa baadhi ya watu mashuhuri duniani.
Akiongea katika kikao cha
waandishi wa habari nje ya afisi yake jijini London, Bwana Cameron amesema kuwa
hahisi tena kuwa mtu muhimu wa kuliongoza taifa hilo kwa ufanisi chini ya
uamuzi kama uliofanywa.
Sauti yake iliibua hisia hasa aliposena naipenda saana
taifa hili na najihisi vizuri kuliongoza muda huo wote.
Bwana Cameron amesema kuwa kauli
ya wengi sharti isikizwe japo hafahamu kwanini Waingereza walichukua uamuzi
kama huo ilhali taifa hilo lilikuwa linaufanisi mkubwa sana ndani ya EU.
Cameron akiwa ameandamana na
mkewe amesema bila shaka sasa utawala mpya unahitajika utakaoweza kutathmini
mbinu na mkataba wa kujiondoa kutoka kwa muungano huo wa bara Ulaya.
0 comments:
Post a Comment