Mchezaji wa Sweden ameonyeshwa kadi nyekundu baada ya mwamuzi kumtuhumu kuwa alifanya vitendo visivyokuwa vya ‘kiungwana’ na ‘kiuanamichezo’ uwanjani.
Adam Lindin Ljungkvist anayeichezea
Pershagens SK, alikuwa uwanjani katika mchezo dhidi ya kikosi cha akiba cha
Jarna SK kwenye mchezo wa Ligi Daraja la Saba Sweden.
Hata hivyo beki huyo wa kushoto
alionyeshwa kadi ya pili ya njano iliyomtoa uwanjani dakika ya 93, baada ya
kupumua akiwa karibu na mwamuzi.
“Nilikuwa na mchafuko wa tumbo, hivyo
nikajikuta nimeshaponyokwa,” alisema nyota huyo wa miaka 25 alipozungumza na
Lanstidningen Sodertalje.
“Nilimuuliza mwamuzi, ‘hivi,
siruhusiwi kupumua hata nikiwa nimebanwa?’ ‘Hapana,’ alinijibu…
Sikuelewa, lakini labda alidhani
nilifanya hivyo mkononi na kumrushia puani. Lakini sikufanya hivyo.”
“Nilizungumza na mwamuzi na
nikamwambia sikufanya makusudi bali ilikuwa ni mchafuko wa tumbo.”
0 comments:
Post a Comment