Baba wa miaka
28 nchini Marekani amenyoa kichwa chake na kuweka mchoro wa tattoo, unaofanana
na kovu la kichwa cha mwanawe aliyefanyiwa upasuaji.
Josh Marshall ambaye anatoka Kansas aliingia katika shindano
la kila mwaka, linaloendeshwa na shirika la hisani kuhusu saratani ya watoto na
kushinda taji la #BestbaldDad {baba mwenye kipara kizuri} wikendi iliopita.
Akikiri aliandika: Mimi na mwanangu katika hafla ya St.
Baldtricks huko Wichita Kansas.
Niliwekwa tatoo ya kovu la mwanangu ili kuimarisha motisha
yake.
Shindano hilo huwashirkisha watu wa familia na marafiki wa
mtoto aliye na saratani.
Mwanawe
alipatikana na uvimbe katika ubongo mnamo mwezi Machi.
''Mwanangu alikuwa na wasiwasi mwingi baada ya kufanyiwa
upasuaji,alijihisi kama hayawani'',alisema Josh Marshal.
0 comments:
Post a Comment