Nahodha na kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Stephen
Keshi (54) amefariki
dunia mapema leo jijini Benin katika jimbo la Edo State.
Msiba huu umekuja ikiwa ni mwaka
mmoja umepita tangu mwanasoka huyo ampoteze mkewe, Kate Keshi, baada ya kuugua
saratani kwa muda mrefu.
Keshi atakumbukwa kuwa miongoni mwa
wanasoka wa kipekee kabisa nchini Nigeria kwani amewahi kutwaa kombe la Mataifa
ya Afrika akiwa mchezaji na kama kocha wa kikosi cha Super Eagle.
“Keshi hakuwa mgonjwa kabisa,
hajawahi kuonyesha dalili zozote za ugonjwa, lakini tunahisi kifo
kimesababishwa na msongo wa mawazo mara baada ya kifo cha mkewe,” mmoja wa
marafiki wa Keshi ameliambia TheCable.
Keshi alizaliwa Januari 23, 1962 huko
Azare katika jimbo la Bauchi na kuanzia soka lake katika timu ya ACB Football
Club, baadaye akajiunga na klabu za New Nigeria Bank, Stade d’Abidjan, Africa
Sports, Lokeren, Anderlecht na RC Strasbourg.
0 comments:
Post a Comment