Sherehe
ya kila mwaka ya kula mbwa imeanza jana kusini mwa taifa la China licha ya
pingamizi kutoka katika taifa hilo na ugenini
Takriban mbwa Elfu 10 na paka kadhaa
wanatarajiwa kuuawa na kuliwa, wakati wa sherehe hiyo ya siku kumi inayofanyika
Yulin.
Wanaharakati wanasema kuwa hafla
hiyo ina ukatili huku wale wanaotaka sherehe hiyo kupigwa marufuku
wakiandikisha saini milioni 11.
Mamlaka ya eneo hilo inasema kuwa sherehe hiyo haiungwi
mkono moja kwa moja na serikali lakini hufanywa na wafanyibiashara wa
kibinafsi.
Sherehe hiyo ya mlo wa nyama ya
mbwa huwaleta pamoja watu wengi, katika eneo la Yulin ili kujichagulia nyama ya
mbwa, matunda na vinywaji.
Utamaduni wa kula
nyama ya mbwa ulianza miaka 500 iliopita nchini China, Korea Kusini pamoja na
mataifa mengine, ambapo wengi wanaamini mlo huo huondoa joto mwilini wakati wa
majira ya kiangazi.
0 comments:
Post a Comment