Kijana Baraka Joshua (23) inayedaiwa alikuwa
akiishi na nyani baada ya kuzaliwa na
kutupwa porini mkoani Shinyanga takriban
miaka minane iliyopita, amepandishwa kizimbani Mahakama ya Wilaya ya Ilala,
kujibu mashtaka ya kumbaka na kumlawiti mtoto wa miaka tisa.
Alifikishwa
mahakamani hapo jana na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali, Florida
Wenceslaus. Alidai Mei 17 eneo la Shule ya Msingi Tabata Kimanga,mshtakiwa
alitenda makosa hayo dhidi ya mtoto ambaye alikuwa anasoma katika shule hiyo.
Mshtakiwa huyo alikana mashtaka na kurudishwa
rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Hakimu Catherine Kiyoja aliahirisha kesi hiyo
hadi Juni 26, ikapotajwa tena.
Awali mshtakiwa
anadaiwa alikuwa anaishi na nyani kabla hajachukuliwa na askari wa wanyamapori
baada ya kumfuatilia kwa karibu.
0 comments:
Post a Comment