Vyombo vya habari vya Marekani vilibashiri Clinton atakuwa na
wajumbe wa kutosha kuwa chaguo
la Democratic, katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika mwezi Novemba.
Pia vyombo hivyo vya habari vya Marekani vilisema Clinton tayari
ana wajumbe elfu 2 mia 3 na 83, wanaomuunga mkono ambao aliwahitaji ili kupata
uteuzi wa chama.
Hii inajumuisha wajumbe wakuu ambao wapo
huru, kumuunga mkono mgombea yeyote lakini tayari wameahidi kumuunga mkono
Clinton.
Mgombea mtarajiwa wa urais kwa chama cha
Republican Donald Trump, amemshambulia vikali anayeonekana mpinzani wake kutoka
chama cha Democratic Hillary Clinton siku ya Jumanne, akimshutumu kwa kuuza
fursa kwa wizara ya mambo ya nje ya Marekani wakati alipokuwa waziri wa mambo
ya nje.
Trump alitoa maneno makali alisema Clinton na mume wake Rais wa
zamani wa Marekani Bill Clinton wamegeuza siasa kujinufaisha binafsi.
Trump alizungumza katika usiku ambao Hillary Clinton, ameweka
historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kupata uteuzi usio rasmi wa chama ili
kuwania urais, baada ya uchaguzi wa awali katika majimbo sita uliofanyika siku
ya Jumanne.
0 comments:
Post a Comment