Watafiti
wanaoendesha uchunguzi katika eneo la Ice land, wanaamini kuwa wanaweza
kupunguza
hewa chafu inayochafua mazingira kwa kunasa hewa ya sumu ya carbon
dioxide, na kuigeuza kuwa mawe.
Wanasayansi hao waliyeyusha hewa
hiyo ndani ya maji,kwa kupuliza mchanganyiko wake ardhini ambako ilichanganyika
na madini ya volcano, na kuunda mawe yanayofanana na chokaa.
Wanasayansi hao wamesema mfumo
huo unaweza kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya viwango vya joto duniani, kwa
sababu mawe ya volcano inayohitajika kugeuza gesi hiyo yanapatikana kote
duniani.
Utafiti huo wa miaka miwili
uligharimu takriban dola milioni 10.
Wanapendekeza kuwa hiyo itakuwa
njia dhabiti ya kupambana na tabia nchi japo itagharimu pesa nyingi.
Mradi huo unaotambuliwa kama
CarbFix, unaweza kunasa hewa ya sumu kutoka angani na kuipenyeza kupitia kwenye
mabomba na maji hadi ardhini.
Shughuli hiyo inakamilika kwa
asilimia 95% ya hewa hiyo kuganda na kuwa jiwe.
0 comments:
Post a Comment