Mkazi wa Njiapanda ya Himo mkoani Kilimanjaro Daniel Mshana (41),
amehukumiwa
kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na kosa la kufanya
ngono na binti yake wa kumzaa.
Suala hilo liligunduliwa na walimu
katika shule aliyokuwa akisoma mtoto huyo mwenye umri wa miaka tisa, baada
kumuona siyo mchangamfu na ufaulu wake darasani kuanza kuporomoka.
Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa
mahakamani baada ya mtoto huyo kuonyesha hali hiyo, mwalimu wa darasa alimhoji
na ndipo alipoeleza mkasa mzima na suala hilo kufikishwa polisi.
Mshtakiwa alikuwa akiishi nammtoto
wake huyo baada ya kutengana na mkewe, ambaye aliondoka na watoto wawili wadogo
na kumwacha binti huyo na baba yake.
Hukumu hiyo ilitolewa Ijumaa
iliyopita na Hakimu Mkazi wa Mkoa Kilimanjaro Anthony Ngowi, aliyesema kitendo
alichokifanya mshtakiwa ni kibaya kisichopaswa kufumbiwa macho na jamii.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu Ngowi amesema
ushahidi wa mashahidi sita akiwamo mtoto mwenyewe, daktari na walimu
umeithibitishia Mahakama kuwa Mshana alitenda kosa hilo.
0 comments:
Post a Comment