Friday 27 May 2016

MTOTO MZITO ZAIDI AZALIWA INDIA…!!!

Mwanamke mmoja nchini India amejifungua mtoto wa uzani wa kilo 6.8, ambaye madaktari
wanasema huenda akawa mtoto mwenye uzani wa juu zaidi kuwahi kuzaliwa nchini humo.

Mtoto huyo ana uzani sawa na mtoto wa umri wa miezi sita.
Nchini humo watoto wengi huzaliwa na uzani wa kadiri wa kilo 2.5 mpaka 3.5.
Mamake Nandini 20 alijifungua kupitia upasuaji katika jimbo la Karnataka, kusini mwa nchi hiyo.
Visa vya watoto kuzaliwa na uzani wa juu kupindukia sana, hutokana na mama kuugua kisukari lakini madaktari wamebaini Nandini hana tatizo hilo.
Rekodi ya mtoto mwenye uzani wa juu zaidi India inashikiliwa na mvulana aliyezaliwa na Firdous Khatun jimbo la Uttar Pradesh Novemba 2015.
Mvulana huyo alikuwa na uzani wa kilo 6.7.

Rekodi ya dunia inashikiliwa na mvulana aiyezaliwa na Carmelina Fedele eneo la Aversa Italia, mwezi Septemba 1955 ambaye alikuwa na uzani wa kilo 10.2.

0 comments:

Post a Comment