Monday 9 May 2016

ABIRIA 31 WA ETIHAD WANUSURIKA KIFO..!!

Watu 31 wamenusurika kifo baada a ndege ya Etihad EY 474 waliyokuwa wakisafiria kutoka Abu
Dhabi kuelekea Jakarta kupata hitilafu ikiwa angani.
Msemaji wa shirika hilo aliliambia Shirika la Habari la AFP kwamba, abiria tisa kati ya hao walijeruhiwa na kulazwa hospitalini nchini Indonesia.
Alisema ajali hiyo ilitokea muda mfupi baada ya ndege hiyo kuruka ikitokea Indonesia.Hali hiyo ilisababisha tafrani kwa abiria ambao baadhi yao walipata majeraha kutokana na mshtuko.
Alisema wataalamu wa shirika hilo walikwenda Indonesia kwa ajili ya uchunguzi wa ndege hiyo ili kubaini tatizo.
Vilevile walikutana na wanafamilia kadhaa wa majeruhi na kuthibitisha kuwa shirika lao litagharimia matibabu.


Rais wa Shirika la Ndege la Etihad na Mkurugenzi Mkuu James Hogan alisema: “Rubani wetu na wafanyakazi wa ndege wanapaswa kupongezwa kwa utulivu wao na namna ambavyo walivyoshughulikia tukio hilo na huduma waliyoionyesha kwa abiria japo kuwa abiria wachache walijeruhiwa,’’ alisema na kuiongeza: “Ni ushahidi wa mafunzo ya kiwango cha juu yanayotolewa kwa wafanyakazi wetu,” alisema.

0 comments:

Post a Comment