Thursday 12 May 2016

WALIMU WALIPWA VIFARANGA BADALA YA MSHAHARA..!!

Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa.

Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan, wamekua wakitoa vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo.
Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani Radio Ozodlik, kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka.
Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema kuwa,hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni lakini wanataka pesa zao.
Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni.
Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari, na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi.
Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka kadhaa sasa, hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni.
Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuuTashkent, walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

0 comments:

Post a Comment