Thursday 12 May 2016

UTAFITI:ASILIMIA 25 YA WANAWAKE WAJAWAZITO HUTOA MIMBA…!!

Mwanamke mmoja kati ya wanne waja wazito hutoa mimba kila mwaka, takwimu kutoka shirika la
afya duniani na taasisi ya Gutt macher zinaashiria.
Ripoti hiyo kutoka jarida la Lancet inasema kuwa, visa milioni 56 vya utoaji mimba hufanyika kila mwaka, kiwango kilicho juu kuliko ilivyodhaniwa.
Watafiti wanakiri kuwa viwango hivyo vimeimarika katika nchi nyingi tajiri, lakini wanaonya kuwa linaficha ukosefu wa mabadiliko katika maeneo maskini katika miaka 15 iliopita.
Wanasayansi wanasema idadi ya visa vya utoaji mimba kila mwaka, vimeongezeka kutoka milioni 50 kwa mwaka kati ya mwaka 1990-1994 hadi milioni 56 kwa mwaka kati ya 2010-2014.
Ongezeko hilo linashuhudiwa zaidi katika nchi zinazoendelea, chanzo kikuu kikiwa ni ongezeko la idadi ya watu na haja ya kuwa na familia ndogo.
Hesabu inaonyesha kwamba wakati visa vya utoaji mimba vinasalia kama vilivyo katika mataifa maskini, katika maeneo tajiri visa hivyo vimeshuka kutoka wanawake 25 hadi 14 kati ya wanawake 100 walio katika umri wa kuzaa.
Amerika kusini imetajwa kuwa kati ya wanawake 3 mmoja hutoa mimba, kiwango kilicho juu kuliko eneo lingine duniani.


0 comments:

Post a Comment