Monday 9 May 2016

MIFUKO 800 YA SUKARI YAKAMATWA…!!

Mapambano  kati ya vyombo vya dola na wafanyabiashara wanaodaiwa kuficha sukari  yameendelea
maeneo mbalimbali nchini huku mifuko ya bidhaa hiyo ikikamatwa mkoani Mwanza.
Taarifa kutoka mkoani Mwanza zinasema Kikosi cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa  huo, kimekamata mifuko 800 kati ya 1,200 ya kilo 50  ambayo  ilikuwa ikishushwa kwenye ghala la mfanyabiashara mmoja kwa ajili ya kufichwa.
Sukari hiyo ilikamatwa juzi   jioni katika Mtaa wa Rufiji, Mwanza ikiwa kwenye gari   ya Scania  namba    T 200 BSV  na tela lake   namba   T 601 DFM, ikiwa limeegesha katika ghala la Adam Michael Balenga.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Augustine Senga alisema baada ya kukamatwa sukari hiyo  mhusika  alidai ilikuwa imetoka Kampuni ya Al Naem Enterprise Ltd ya  Tabata, Dar es Dar es Salaam.
“Tumekamata sukari mifuko 800 ya kilo 50. Hii ilikuwa ikiuzwa kwa siri nyumbani kwa mfanyabiashara, wakati tunakamata tayari kiasi kingine cha mifuko 400 ilikuwa imekwisha kuuzwa,” alisema Senga.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema kikosi kazi kimeanza kazi vizuri na  bado kinafuatilia nyendo za baadhi ya wafanyabiashara ambao wanaonekana kuanza kutoa sukari na kuiuza kwa siri baada ya agizo la Rais Dk. John  Magufuli.

0 comments:

Post a Comment