Thursday 12 May 2016

MWANAMKE AFUTWA KAZI KWA KUTOVAA VIATU VYA JUU..!!

Karani mmoja wa kupokea wageni mjini London, alilazimika kurudi nyumbani baada ya kukataa
kuvaa viatu vyenye visigino virefu (High hills) imebainika.

Mfanyakazi huyo wa kampuni ya Temp Nicola Thorp mwenye umri wa miaka 27 kutoka Hackney, amewasili katika kampuni moja inayoshughulikia maswala ya kifedha PwC, kabla ya kuarifiwa kwamba anahitajika kuvaa viatu vyenye visigino vya nchi 2 hadi 4.
Alipokataa na kulalamika kwamba mbona wenzake wa kiume hawakutakiwa kuvaa hivyo, alitakiwa kurudi bila ya mshahara.

Kampuni ya Portico imesema kuwa iliweka sheria hizo kwa wafanyikazi wanaokabidhiwa PwC, na imesema kuwa haitaondoa sheria hiyo.

0 comments:

Post a Comment