Wednesday 4 May 2016

SERIKALI YAMFUNGIA SNURA, WIMBO WA CHURA…!!

Wizara ya Habari, utamaduni, sanaa na michezo imefungia video na wimbo wa "chura" ulioimbwa na msanii Snura Mushi.

Msanii huyo pia amefungiwa kufanya maonyesho ya wazi kwa sababu imebainika kwamba hana kibali kutoka Basata kinachomtambua kama msanii.
Msemaji wa wizara hiyo, Zawadi Msalla amesema wizara ilikaa na Basata, TCRA, bodi ya filamu na Snura mwenyewe na kufikia uamuzi wa kuufungia wimbo huo kwa sababu unadhalilisha, hauna maadili na unakiuka haki za binadamu.
Msalla amesema wizara imemtaka msanii huyo kuutoa wimbo huo kwenye mtandao wa YouTube na chombo chochote hakitakiwi kupiga wimbo wala kuonyesha video hiyo.


"Mtu yoyote atakayeendelea kusambaza wimbo au video ya chura atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ya makosa ya mtandao. Kwa hiyo wananchi wajihadhari katika hilo," amesema Msalla.

0 comments:

Post a Comment